Guardiola |
BAYERN,
Ujerumani
MKURUGENZI
Mkuu wa Bayern Munich, Karl-Heinz Rummenigge alishindwa kutoa jibu la moja kwa
moja wakati alipoulizwa juu ya taarifa kwamba wanataka kumchukua kocha Pep
Guardiola, lakini akasema kwamba kocha Jupp Heynckes ataendelea kuinoa timu yao
hadi mwishoni mwa mwaka 2012.
Hatma ya
Heynckes katika kuiongoza Bayern iko shakani baada ya kumaliza katika nafasi ya
pili kwenye michuano mitatu msimu uliopita, na kocha wa zamani wa Barca amekuwa
akihusishwa na klabu hiyo.
Lakini,
akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari kumtambulisha Matthias Sammer
kuwa mkurugenzi mpya wa michezo wa Bayern, Rummenigge alifichua kwamba klabu
yao haitakurupuka kuhusiana na hatma ya kocha wao wa sasa.
"Tutafikiria
kwa utulivu. Hamtapata maelezo yoyote kutoka kwetu kuhusiana na jambo hili
kabla ya krismasi," Rummenigge aliwaambia waandishi wa habari.
"Baada
ya hapo ndipo tutakapokaa na kuzungumza.
"Pep
Guardiola? Hata mimi nimesoma habari hiyo, lakini hakuna yeyote kutoka Bayern
ameithibitisha."
No comments:
Post a Comment