Wednesday, July 4, 2012

BALOTELLI AHOFIA KUBAMBIKIWA MTOTO

Hapa Balotelli anatembea 'zero distance' kabla ya kuzinguana na Rafaella

Balotelli na Rafaella

Twende mpenzi...! Balotelli akiwa na Rafaella enzi hizo wakiwa na mapenzi ya kugandana kama luba.

Haa..haa...haaaa...pendeza eeee!

Balotelli na mpenzi wake wa zamani, Rafaella

Balotelli na Rafaella wakikatiza mitaa baada ya kutoka 'shopping' kabla hawajamwagana

Hapa ni enzi za mapenzi motomoto kati ya Balotelli na Rafaella


MILAN, Italia
MARIO Balotelli anataka achukuliwe vipimo vya vinasaba (DNA) baada ya mwanamke wa Kiitaliano, Raffaella Fico kudai jana kwamba ana mimba ya straika huyo wa klabu ya Manchester City.

Raffaella ambaye ni mpenzi wa zamani wa mchezaji huyo wa timu ya taifa ya Italia, aliliambia jarida la Chi kwamba alimpa Balotelli taarifa za ujauzito wake Alhamisi baada ya mechi yao ya nusu fainali ya Euro 2012 dhidi ya Ujerumani, akimueleza zaidi kuwa ana mimba yake ya miezi minne.

Balotelli sasa ametoa taarifa kwa vyombo vya habari inayodai kwamba hakusudii kukwepa majukumu, lakini anataka wachukuliwe vipimo vya DNA kuthibitisha kama kweli yeye ndiye baba wa mtoto huyo.

"Ingawa sipendi kuzungumzia mambo yangu binafasi hadharani, nafikiri katika hili nina wajibu wa kuweka wazi, kwa mara ya kwanza na ya mwisho, kuhusiana na mahusiano yangu na Raffaella Fico," straika huyo mwenye miaka 21 alieleza.

"Uhusiano wetu ulifikia ukomo mwanzoni mwa Aprili na tangu wakati huo hatujaonana, wala kuwasiliana.
"Sina chochote cha kufuatilia maisha yake na Raffaella hana cha kufuatilia juu ya maisha yangu.

"Raffaella anatambua vyema kwamba tangu tulipoachana, sikuwa na sina nia ya kurudiana naye.
"Lakini kwa sababu ya kile kilichokuwapo kati yetu, sikutaka kuzungumzia suala hili, hata pale pale palipokuwa na vitu vya uongo vilivyokuwa vikisemwa na kaundikwa kuhusiana na hili.

"Siku chache zilizopita nilijulishwa na watu wengine kwamba Raffaella ana mimba. Kwa sababu hii, niliamua kuwasiliana naye na baada ya kumuuliza ndipo aliponithibitishia kuwa ni kweli.

"Nimehuzunishwa sana. Sidhani kama ni kawaida kutojulishwa hadi kufikia mwezi wa nne (kuhusiana na mimba).
"Sielewi ni kwanini hakuniambia mapema jambo kubwa kama hili.

"Nitabeba majukumu yote wakati nitakapokuwa na ushahidi kwamba kweli ana mimba yangu."
Balotelli aliendelea: "Vilevile, inanikera kuona kwamba tayari ameshaanza kusaka fedha kwa kuuza mahojiano yake juu ya habari hii na picha.

"Nadhani kwamba Rafaella tayari ameshakuwa maarufu na hivyo hahitaji kutumia habari hii kwa lengo la kujitangaza.

"Hii ni mara ya kwanza na ya mwisho kwangu kuzungumzia suala hili hadharani na hivyo sikusudii kujibu chochote kuhusiana na kile kinachosemwa au kuandikwa na Raffaella."

Fico amedai kwamba Balotelli, aliyefunga mara mbili na kuisaidia Italia kuibuka na ushindi wa 2-1 dhidi ya Ujerumani, alijawa na furaha kusikia kwamba anatarajia kupata mtoto.

No comments:

Post a Comment