Wednesday, July 25, 2012

ARSENAL YAKARIBIA KUMSAJILI CAZORLA

Picha iliyosambazwa na Chama cha Soka cha Hispania, ikimuonyesha Santi Cazorla wa timu ya taifa ya Hispania akipozi na kombe baada ya timu yake kutwaa ubingwa wa Mataifa ya Ulaya (Euro) 2012 kwa kuifunga Italia katika fainali akiwa katika ndege waliyopanda wachezaji wa timu ya taifa ya Hispania wakati wakirejea nyumbani mjini Madrid Jula 2, 2012.
Santi Cazorla wa timu ya taifa ya Hispania akikimbia na mpira wakati wa mechi yao ya robo fainali ya UEFA Euro 2012 dhidi ya Ufaransa kwenye Uwanja wa Donbass Arena mjini Donetsk, Ukraine Juni 23, 2012. Hispania ilishinda 2-0, magoli yote yakifungwa na Xabi Alonso.
Santi Cazorla (kulia) wa timu ya taifa ya Hispania akimpongeza Xabi Alonso baada ya kufunga goli wakati wa mechi yao ya robo fainali ya UEFA Euro 2012 dhidi ya Ufaransa kwenye Uwanja wa Donbass Arena mjini Donetsk, Ukraine Juni 23, 2012. Hispania ilishinda 2-0, magoli yote yakifungwa na Alonso.

ARSENAL wanakaribia kukamilisha usajili wa kiungo wa timu ya taifa ya Hispania Santi Cazorla baada ya mkali huyo kuafiki malipo binafsi na klabu hiyo.

Kiungo huyo wa Malaga anatarajiwa kukamilisha uhamisho wake wa kutua London Kaskazini katika wiki chache zijazo, mwaka mmoja baada ya kutakiwa kwa mara ya kwanza na Arsene Wenger.

Arsenal imeweka mezani ada ya uhamisho ya paundi milioni 15.6 kwa ajili ya mchezaji huyo ambaye ni miongoni mwa wenye vipaji vikubwa katika La Liga na dili linatarajiwa kukamilika kutokana na dhamira ya mchezaji huyo kuhama.

Cazorla alijiunga na Malaga Juni mwaka jana akitokea Villarreal - ambao baadaye walishuka daraja - lakini amekuwa katika malumbano na klabu yake kutokana na kutolipwa mishahara yake.

Hali ya kifedha si njema katika klabu hiyo inayomilikiwa na Waarabu, ambayo inadawiwa kodi kubwa na serikali ya Hispania, pamoja na madeni kibao ambayo hayajalipwa kuhusiana na uhamisho wa wachezaji.

Na sasa gazeti la The Guardian limesema kuwa kiungo huyo mwenye umri wa miaka 27 atakuwa mchezaji wa kwanza mwenye jina kubwa kutimka klabuni hapo ili kusaidia kulipa madeni.

Cazorla, ambaye alifunga 'frikiki' nne msimu uliopita, alicheza takribani katika kila katika kiungo na ushambuliaji, na itakuwa nyota wa tatu kutua Arsenal katika kipindi hiki cha usajili, baada ya Lukas Podolski na Olivier Giroud.

No comments:

Post a Comment