Tuesday, June 19, 2012

VIDEO MPYA YA BANANA Ft. DOGO ASLAY  YATOKA

Banana Zorro (kulia) akiimba pamoja na baba yake mzazi Zahir Ali Zorro wakati wa moja ya maonyesho ya B-Band.

Na Ramadhani Mbwaduke
NYOTA wa muziki wa kizazi kipya nchini na mkurugenzi wa bendi yake mwenyewe inayokwwenda kwa jina la B-Band, Banana Zahir Zorro, ameachia video ya wimbo wake mpya wa ‘Nunda’ aliouimba akimshirikisha  msanii anayeinukia vyema Dogo Aslay.
Banana ameiambia Blog ya STRAIKA kuwa wimbo huo umerekodiwa na studio ya Soundcrafters wakati video imefanywa na kampuni inayoaminika kuwa bora zaidi nchini ya Visual Lab chini ya muongozaji Adam Juma.  
“Ni wimbo mzuri sana, nina furaha kwamba mashabiki wangu wanaweza kupata kitu kipya baada ya kusubiri kwa muda kidogo,” amesema Banana.
Muimbaji huyo anayetamba na nyimbo kama ‘Nzela’, ‘Mama Kumbena’ na ‘Zoba’, amesema mambo wimbo huo mpya na nyingine zake zote zinapatikana katika maonyesho ya B-Band kila wiki.
B-Band ambayo pia inamjumuisha baba yake mzazi, gwiji wa muziki nchini Zahir Ali Zorro, inatumbuiza  kila Alhamisi hutumbuiza kwenye ukumbi wa Q-Bar uliopo Oysterbay jijini Dar es Salaam,  Ijumaa wanapatikana Arabella, Masaki jijini Dar es Salaam wakati siku ya Jumamosi huitumia kutumbuiza kwenye maeneo mbalimbali kulingana na mialiko.

No comments:

Post a Comment