JUMA NATURE, ROMA, MWASITI KUPAMBA AIRTEL Supa5 MWANZA
Na Mwandishi Wetu
TAMASHA la burudani maalum kwa ajili ya kuitambulisha huduma ya Airtel Supa5 mikoani litaendelea mwishoni mwa wiki hii kwa burudani ya aina yake katika viwanja vya wazi vya Furahisha vilivyopo jijini Mwanza.
Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde alisema lengo la kuunganisha utambulisho huo na burudani ni kuwavutia vijana na wateja wengi kuhudhuria na kujifunza faida lukuki za SUPA5 ili waitumie zaidi.
"Tamasha linafanyika kwa siku mbili mfululuzizo ambapo siku ya Jumamosi tunatoa fursa kwa wasanii chipukizi kujitokeza kwa wingi kuonyesha vipaji vyao sambamba na kupata huduma ya Airtel SUPA5.
"Jumapili itakuwa uzinduzi kamili ambapo wasanii wakubwa watatoa burudani bure, akiwemo Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, Mwasiti a.k.a Soja, Roma Mkatoliki, watatoa burudani kali kwa wateja watakaohuduria tamasha hilo la bure.
Huduma ya Airtel SUPA5 ilizinduliwa rasmi siku za karibuni jijini Dar es Salaam na kisha kufuatiwa na matamasha ya burudani ya bure katika mikoa ya Dodoma, Morogoro, Iringa, Arusha.
Wasanii nyota waliokwishapamba majukwaa ya Airtel SUPA5 hadi sasa ni Chege, Temba, Fid Q, Mwasiti, Godzillah, kundi la Tip Top Connection akiwemo Madii, Tundaman, Richard na Dogo Janja na bendi maarufu jijini ya Mashujaa ikiongozwa na muimbaji nyota Chaz Baba.
--------------
No comments:
Post a Comment