Tuesday, June 19, 2012

JUMA NATURE, ROMA, MWASITI KUPAMBA AIRTEL Supa5 MWANZA


Wasanii wa kundi la kudansi la Kinoko, maarufu kama Comedy Dance, wakifanya vitu vyao wakati wa Tamasha la Airtel Supa5 katika viwanja vya NMC mjini Arusha wiki iliyopita. Wasanii hao watakuwepo pia katika tamasha hilo jijini Mwanza wikiendi hii.

Rapa Juma Nature wa kundi la Wanaume Halisi (kushoto) akitumbuiza mbele ya umati wa mashabiki wakati wa tamasha maalum la kuitambulisha huduma ya Airtel Supa5 kwenye viwanja vya NMC mkoani Arusha mwishoni mwa wiki. Nature atakuwepo mjini Mwanza wikiendi hii katika mwendelezo wa tamasha hilo.

Mwasiti (kulia) akitumbuiza mashabiki wakati wa tamasha maalum la kuitambulisha huduma ya Airtel Supa5 kwenye viwanja vya NMC mkoani Arusha mwishoni mwa wiki. Mwasiti pia atakuwepo mjini Mwanza wikiendi hii katika mwendelezo wa tamasha hilo.

Na Mwandishi Wetu
TAMASHA la burudani maalum kwa ajili ya kuitambulisha huduma ya Airtel Supa5 mikoani litaendelea mwishoni mwa wiki hii kwa burudani ya aina yake katika viwanja vya wazi vya Furahisha vilivyopo jijini Mwanza.

Afisa Uhusiano wa Airtel, Jane Matinde alisema lengo la kuunganisha utambulisho huo na burudani ni kuwavutia vijana na wateja wengi kuhudhuria na kujifunza faida lukuki za SUPA5 ili waitumie zaidi.

"Tamasha linafanyika kwa siku mbili mfululuzizo ambapo siku ya Jumamosi tunatoa fursa kwa wasanii chipukizi kujitokeza kwa wingi kuonyesha vipaji vyao sambamba na  kupata huduma ya Airtel SUPA5.

"Jumapili itakuwa uzinduzi kamili ambapo wasanii wakubwa watatoa burudani bure, akiwemo Juma Nature na kundi zima la Wanaume Halisi, Mwasiti a.k.a Soja, Roma Mkatoliki, watatoa burudani kali kwa wateja watakaohuduria tamasha hilo la bure.

Huduma ya Airtel SUPA5 ilizinduliwa rasmi siku za karibuni jijini Dar es Salaam na kisha kufuatiwa na matamasha ya burudani ya bure katika mikoa ya Dodoma, Morogoro, Iringa, Arusha.

Wasanii nyota waliokwishapamba majukwaa ya Airtel SUPA5 hadi sasa ni Chege,  Temba, Fid Q, Mwasiti, Godzillah, kundi la Tip Top Connection akiwemo Madii, Tundaman, Richard na Dogo Janja na bendi maarufu jijini ya Mashujaa ikiongozwa na muimbaji nyota Chaz Baba.

--------------



No comments:

Post a Comment