BINTI WA BOBBY BROWN AKACHA HARUSI YA BABA YAKE
WAKATI wa mapumziko
mafupi ya ziara ya kundi la New Edition,
msanii Bobby Brown aliamua kumuoa mpenzi wake wa ‘long taim kitambo’, Alicia
Etheredge, tukio lililofanyika Honolulu, juzi Jumatatu.
Cha
kusikitisha, ingawa tukio hilo lilikuwa ni la kifamilia, binti wa gwiji huyo, Bobbi
Kristina Brown hakushiriki tukio hilo.
Brown, 43, mkali
wa muziki wa R&B aliyemchumbia Etheredge tangu mwaka 2010, alisema "Nimekubali"
mbele ya ndugu na marafiki, wakiwemo wanawe wakubwa Landon, 23, La'Princia, 22,
na Bobby Jr., 19, na kitinda mimba wake aliyezaa na Etheredge: Cassius, 3.
Bobbi
Kristina, binti yake aliyezaa marehemu Whitney Houston, hakuonekana katika harusi
hiyo.
Taarifa zimedai
kwamba Bobbi Kristina anapiga picha za kipindi chake kipya cha luninga jijini New
York na hivyo ameamua ‘kuipotezea’ harusi ya baba yake.
Imeelezwa
zaidi kuwa hivi sasa, Bobby Brown na binti yake huyo hawapikiki chungu kimoja.
Hata hivyo, licha
ya kutokuwepo kwa Bobbi Kristina, sherehe hizo zilifanyika kama zilivyopangwa.
Bobby alivalia suti iliyokuwa na rangi nyekundu na shati la rangi ya maziwa.
Cassius, aliyeshika
pete ya ndoa, alivalia kama baba yake lakini akaongezea na ‘skafu’ shingoni
mwake. Bobby Jr. alipiga picha nyingi za harusi hiyo, ikiwemo ya mabinti wanne walioshikilia
maua.
Kabla ya kuchumbiana
mwaka 2010 (suala ambalo Bobby alikuwa mkali kila mara alipoulizwa wakati wa
maonyesho yake, wapenzi hao ‘walijirusha’ kwa miaka mitatu na kumzaa Cassius mwaka
2009. Uhusiano wake na Etheredge, ambaye pia ni meneja wake, ndio wa kwanza
uliodumu zaidi baada ya kutalikiana na Houston mwaka 2007.
"Nimefahamiana
na Alicia kwa miaka kadhaa," Bobby aliwahi kusema mwezi uliopita.
"Tulikutana
zamani sana, wakati akijifunza unenguaji. Alikuwa ni miongoni mwa wacheza shoo.
Tukawa pamoja L.A... tukapotezana baada ya mimi kuoa. Lakini mara tu nilipotalikiana
(na Houston), nikaonana naye tena na kuanza naye upya … ni mwanamke bomba. Nampenda
sana. Mapenzi yangu kwake ni makubwa zaidi ya niliyo nayo kwa mtu mwingine
yeyote," alisema Brown.
-------
No comments:
Post a Comment