Tuesday, June 19, 2012

KENYA YAMTIMUA KOCHA KIMANZI, BENCHI LA UFUNDI

Kocha aliyetimuliwa Harambee Stars, Francis Kimanzi.

NAIROBI, Kenya
KENYA imemtimua kocha Francis Kimanzi kutoka ajira yake leo na kutimua pia watu wote wa benchi lake la ufundi kufuatia matokeo mabaya katika mechi zao tatu za kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia na Mataifa ya Afrika.

Timu hiyo ilitoka sare dhidi ya Malawi mjini Nairobi Juni 2 na ikalala kwa Namibia siku nane baadaye katika mechi mbili za kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil.

Kenya kisha walilala 1-0 kwa Togo, na kuzima ndoto zao kucheza fainali za Mataifa ya Afrika 2013.
"Kamati Kuu ya taifa ilifanya mkutano leo na kuamua kuliondoa benchi zima la ufundi mara moja," alisema mwenyekiti wa Shirikisho la Soka la Kenya (FKF), Sam Nyamweya katika taarifa.

"Francis Kimanzi sasa ameteuliwa kuwa mkurugenzi wa ufundi wa muda kuchukua nafasi ya Patrick Naggi ambaye amekuwa afisa mtendaji waFKF."

No comments:

Post a Comment