Friday, May 17, 2013

BIG BROTHER YAREJEA, KUZINDULIWA JUMAPILI MEI 26

Logo mpya ya Big Brother The Chase 2013
Mtangazaji wa Big Brother, IK.


SHOO kubwa zaidi Afrika ya Big Brother imerejea katika msimu wake 8 mara hii ikienda kwa jina la The Chase.

Washiriki 28 kutoka nchi 14 za Afrika watakuwa wakifukuzia sit u zawadi ya kwanza ya dola 300 000 za Marekani lakini pia kupata umaarufu na hata kutafuta wenza. 

Msimu mpya wa Big Brother The Chase utazinduliwa Jumapili Mei 26 na itajumuisha mabadiliko mengo na ‘surprise’ kubwa ambazo zitahitaji washiriki kutumia werevu wao ili kusonga mbele.

Habari nzuri za ziada ni kwamba mburudishaji IK Osakioduwa kwa mara nyingine atarejea kuwa muongozaji wa shindano hilo la mwaka 2013 la The Chase. Amekuwa kipenzi cha mashabiki wengi kote Afrika kutokana na uwezo wake kuzungumza kwa uwazi na washiriki na kuwasaidia kuchukulia poa vipindi vyao vigumu.

Kwa siku 91, shoo hiyo kubwa Afrika itaonyeshwa ‘live’ kwa saa 24 za siku zote 7 za wiki katika channel 197 na 198 za DStv.

No comments:

Post a Comment