Monday, February 4, 2013

SIMBA, JKT RUVU ZAINGIZA MIL. 73.5/-


Watazamaji 12,984 walikata tiketi kushuhudia mechi ya namba 99 ya Ligi Kuu ya Vodacom iliyochezwa jana (Februari 3 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kumalizika kwa sare ya bao 1-1.

Viingilio katika mechi hiyo vilikuwa sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000 ambapo jumla ya sh. 73,532,000 zilipatikana. Kila klabu ilipata mgawo wa sh. 17,443,752.45 ambapo Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 11,216,745.76.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 8,869,704.64, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 5,321,822.78, Kamati ya Ligi sh. 5,321,822.78, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,660,911.39 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 2,069,597.75.

No comments:

Post a Comment