Friday, January 4, 2013

MAELFU WAJITOKEZA KUMZIKA SAJUKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO.... ZITTO KABWE AIBUKA MSIBANI KISHEIKH KWA KANZU NA KIBALAGHASHEE..!

Waombolezaji wakianza harakati za kusafirisha jeneza la marehemu Sajuki kutoka Tabta kuelekea katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo Januari 4, 2013. (PICHA: Kwa Hisani ya issamichuzi.blogspot.com)

Hapa ni wakati wa kusomwa dua kabla jeneza la marehemu Sajuki halijapelekwa katika makaburi ya Kisutu jijini Dar es Salaam leo Januari 4, 2013.

'Sheikh Zitto Kabwe' (wa pili kulia) akiwa na waombolezaji wengine nyumbani kwa marehemu Sajuki, Tabta Bima jijini Dar es Salaam leo kabla ya mazishi kufanyika kwenye makaburi ya Kisutu jijini Dar leo Januari 4, 2013.
Mhe. Zitto Kabwe (mwenye kanzu na barghashia) akikaribishwa msibani na watu wa bongomovie. kulia ni msanii Jissu.(PICHA ZOTE: Kwa Hisani ya issamichuzi.blogspot.com)
Maelfu ya wakakazi wa jiji la Dar es Salaam na maeneo jirani walijitokeza kwa wingi katika eneo la Tabata Bima jijini Dar es Salaam leo kushiriki mazishi ya  msanii nyota wa filamu za Kibongo, Sajuki ambaye hatimaye alizikwa katika makaburi ya Kisutu.

Wasdanii wenzake mbalimbali nyota wa filamu, wanamuziki, viongozi mbalimbali wa kisiasa na wananchi wa kawaida ni miongoni mwa watu waliojitokeza ambapo baada ya swala ya Ijumaa na kisha mwili wa marehemu huyo ambaye jina lake kamili ni Juma Kilowoko, ulsafirishwa kutoka Tabta hadi kwenye makaburi ya Kisutu na kuzikwa kwa kufuata taratibu zote za Kiislamu.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini ambaye pia ni Naibu Katibu Mkuu wa Chadema, Mhe. Zitto Kabwe, ni miongoni mwa wanasiasa kibao walioshiriki mazishi hayo. Zitto ambaye pia ni mkazi wa Tabata na aliyeshiriki kwa kiasi kikubwa harakati za kumchangia Sajuki wakati akiugua kwa kuongoza kampeni maalum akishirikiana na wabnunge wezake kama Ester Bulaya (CCM) na Halima Mdee (Chadema), alionekana kivingine leo ambapo alitupia kanzu na kofia ya balaghashee vilivyomtoa na kuonekana kama sheikh fulani hivi wa ukweee!

No comments:

Post a Comment