Monday, December 24, 2012

DISKO TOTO MARUFUKU KESHO KRISMASI

Kamanda Kova

KAMANDA wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Suleiman Kova amepiga marufuku Disko Toto katika sikukuu ya Krismasi kesho.

Kamanda Kova amesema leo kwamba wameamua kuchukua hatua hiyo kwa lengo la kulinda usalama wa watoto.

Alisema pia kutakuwa na ulinzi wa askari wa miguu, pikipiki, Land Rover na farasi kwa ajili ya kuhakikisha watu wanasherehekea sikukuu hiyo kwa amani.

Hatua hiyo inafuatia matukio kadhaa ya watoto kufariki wakati wakiwa katika kumbi za Disko Toto.

Septemba 2010 watoto wawili walifariki dunia na wengine 12 kujeruhiwa vibaya baada ya kukosa hewa ukumbini walikokuwa wamejazana kusherehekea Sikukuu ya Idd katika ukumbi wa disko wa Luxury Pub ulioko Temeke, jijini Dar es Salaam.

Tukio hilo lilifuatia jingine lililotokea Oktoba mosi mwaka 2008, wakati watoto 19 walipofariki dunia kwa kukosa hewa kwenye ukumbi wa Disco wa Bubbles unaomilikiwa na Shirika la Hifadhi ya Jamii (NSSF) mkoani Tabora.

No comments:

Post a Comment