Thursday, November 8, 2012

MKENYA VICTOR WANYAMA AWEKA HISTORIA, AWAZAMISHA KINA MESSI.... MAN UTD YAZINDUKA NA KUUA 3-1, CHELSEA YASHINDA LICHA YA KUUSAKA KWA TOCHI

Kiatu cha Lionel Messi wa Barcelona kikionekana na jina la mwanae aliyempa jina la THIAGO aliyezaliwa wikiendi iliyopita wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Celtic kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana usiku. Barca walilala 2-1. Mkenya Victor Wanyama alifunga goli moja la Celtic na jingine lilifungwa na yosso mwenye umri wa miaka 18 aliyeingia kutokea benchi,  Tony Watt. Goli la kufutia machozi ya Barca lilifungwa na Messi. Messi sasa amebakisha goli moja kuifikia rekodi ya gwiji wa Brazil, Pele, ya kufunga magoli 75 katika mwaka mmoja. Picha: REUTERS
Lionel Messi wa Barcelona akishangilia goli lake kwa kunyonya kidole gumba kuashiria kuzaliwa kwa mwanae wa kwanza, THIAGO, wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Celtic kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana usiku. Barca walilala 2-1. Mkenya Victor Wanyama alifunga goli moja la Celtic na jingine lilifungwa na yosso mwenye umri wa miaka 18 aliyeingia kutokea benchi,  Tony Watt. Goli la kufutia machozi ya Barca lilifungwa na Messi. Messi sasa amebakisha goli moja kuifikia rekodi ya gwiji wa Brazil, Pele, ya kufunga magoli 75 katika mwaka mmoja. Picha: REUTERS
RVP wewe ni jembeeee... kocha wa Manchester United, Sir Alex Ferguson akiwapa dole wachezaji wake wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu dhidi ya Braga. Man  U ilishinda 3-1 kupitia magoli ya Robin van Persie, Rooney (penalti) na Chicharito.
Mchezaji wa Juventus, Alessandro Matri akimiliki mpira wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Nordsjaelland kwenye Uwanja wa Juventus mjini Turin jana Novemba 7, 2012. Juve walishinda 4-0. Picha: REUTERS
Utadhani siye Pirlo... kiungo 'jembe' la Juventus, Andrea Pirlo akipiga makofi baada ya mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Nordsjaelland kwenye Uwanja wa Juventus mjini Turin jana Novemba 7, 2012. Juve walishinda 4-0. Picha: REUTERS
Mashine hiyo wanayoitaka Chelsea.... Willian wa Shakhatar akishangilia

Willian wa Shakhatar

Kiungo wa BATE Borisov, Alexandr Hleb (katikati) akilindwa na wachezaji wa Valencia, Ricardo Costa (kushoto) na  Fernando Gago wakati wa mechi yao ya Kundi F la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Mestalla mjini Valencia, jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS
Mchezaji wa Shakhtar Donetsk, Tomas Hubschman (kulia) akimbana straika wa Chelsea, Fernando Torres wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS


Kocha wa Chelsea, Roberto di Mateo akitoa maelekezo
Kiungo wa Juventus, Andrea Pirlo (kulia) akimuacha mchezaji wa Nordsjaelland, Mikkel Beckmann wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Juventus mjini Turin jana Novemba 7, 2012. Juve walishinda 4-0. Picha: REUTERS
Beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic akiwania mpira dhidi ya mchezaji wa Shakhtar Donetsk, Razvan Rat wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Winga wa Bayern Munich, Franck Ribery akionyeshwa kadi ya njano kwa kumlalamikia refa wa Romania, Ovidiu Alin Hategan (kulia) wakati akipumzishwa katika mechi yao ya Kundi F la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya dhidi ya Lille mjini Munich Novemba 7, 2012. Bayern ilishinda 6-1. Picha: REUTERS
Straika wa Benfica, Oscar Cardozo akishangilia goli lake la pili dhidi ya Spartak Moscow wakati wa mechi yao ya Kundi G la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Luz mjini Lisbon jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS
Beki wa Chelsea, Branislav Ivanovic akichezewa faulo na Willian wa Shakhtar Donetsk (kulia) wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Straika wa Barcelona, David Villa akijilaumu baada ya kukosa goli dhidi ya Celtic wakati wa mechi yao ya Kundi G la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS
Straika wa Barcelona, Lionel Messi (katikati) akijaribu kushuti golini huku akibanwa na mchezaji wa Celtic, Adam Mathews wakati wa mechi yao ya Kundi G la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS

Oscar Cardozo wa Benfica akishangilia baada ya kutupia
Dah.... umenibania sana leo, siamini!!! Straika wa Barcelona, Lionel Messi (kushoto) akimuangalia kipa wa Celtic, Fraser Forster baada ya kuokoa shuti la Messi wakati wa mechi yao ya Kundi G la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS
Mchezaji wa Celtic, Kelvin Wilson (kulia) akimpa shughuli kiungo wa Barcelona, Cesc Fabregas wakati wa mechi yao ya Kundi G la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow, Scotland jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTER

Messi akishangilia goli lake kwa kunyonya dole gumba akiashiria kuzaliwa kwa mwanae wa kwanza aliyempa jina la Thiago wakati wa mechi yao dhidi ya Celtic.
Sijaona Mkenya kama wewe uwanjani... Kocha wa Celtic, Neil Lennon (kushoto) akimpongeza mmoja wa wafungaji wa Celtic, Mkenya Victor Wanyama, baada ya ushindi wa timu yao dhidi ya Barcelona katika mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow nchini Scotland jana Novemba 7, 2012. Celtic ilishinda 2-1. Picha: REUTERS
Mkenya Victor Wanyama wa Celtic (kushoto) akipongezwa na wenzake baada ya kufunga goli dhidi ya Barcelona wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya jana. Picha: Reuters
Messi akimpiga chenga Wanyama
Winga wa Chelsea, Victor Moses (kushoto) akishangilia na mchezaji wenzake Gary Cahill (kulia) baada ya kufunga goli wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Winga wa Chelsea, Victor Moses (kushoto) akishangilia na mchezaji wenzake Gary Cahill (kulia) baada ya kufunga goli wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Winga wa Chelsea, Victor Moses (katikati) akishangilia na wachezaji wenzake Gary Cahill (kulia) na Juan Mata baada ya kufunga goli wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Winga wa Chelsea, Victor Moses (katikati) akishangilia na wachezaji wenzake Gary Cahill (kulia) na Juan Mata baada ya kufunga goli wakati wa mechi yao ya Kundi E la Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Shakhtar Donetsk kwenye Uwanja wa Stamford Bridge mjini London jana Novemba 7, 2012. Chelsea walishinda 3-2. Picha: REUTERS
Straika wa Manchester United, Wayne Rooney (kushoto) akipongezwa na mchezaji mwenzake Robin van Persie baada ya kufunga dhidi ya Braga wakati wa mechi yao ya Kundi H la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwenye Uwanja wa Manispaa mjini Braga, jana Novemba 7, 2012. Man Utd ilishinda 3-1. REUTERS
Yosso wa Celtic, Tony Watt (kulia) akifunga goli dhidi wa kipa wa Barcelona, Victor Valdes wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow nchini Scotland jana Novemba 7, 2012. Celtic ilishinda 2-1. Picha: REUTERS
Kocha wa Celtic, Neil Lennon, akishangilia ushindi wa timu yake dhidi ya Barcelona baada ya mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow nchini Scotland jana Novemba 7, 2012. Celtic ilishinda 2-1. Picha: REUTERS
Wachezaji wa Celtic wakimpongeza Tony Watt (32) kwa goli alilofunga wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Barcelona kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow nchini Scotland jana Novemba 7, 2012. Celtic walishinda 2-1. Picha: REUTERS
Nimetishaaa.... yosso wa Celtic, Tony Watt (kulia) akishangilia goli lake wakati wa mechi yao ya Ligi ya Klabu Bingwa dhidi ya Barcelona kwenye Uwanja wa Celtic Park mjini Glasgow nchini Scotland jana Novemba 7, 2012. Picha: REUTERS

Matokeo na misimamo ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya baada ya mechi za jana na juzi:
    KUNDI E
    Juventus         4 Nordsjaelland    0
    Chelsea          3 Shakhtar Donetsk 2
           
    Msimamo            P  W  D  L  F  A  Pts
    Shakhtar Donetsk   4  2  1  1  7  5  7
    Chelsea            4  2  1  1 10  6  7
    Juventus           4  1  3  0  8  4  6
    Nordsjaelland      4  0  1  3  1 11  1

KUNDI F Valencia 4 BATE Borisov 2 Bayern Munich 6 Lille 1 Msimamo P W D L F A Pts Bayern Munich 4 3 0 1 10 5 9 Valencia 4 3 0 1 10 4 9 BATE Borisov 4 2 0 2 8 9 6 Lille 4 0 0 4 2 12 0
KUNDI G Benfica 2 Spartak Moscow 0 Celtic 2 Barcelona 1 Msimamo P W D L F A Pts Barcelona 4 3 0 1 8 5 9 Celtic 4 2 1 1 6 5 7 Benfica 4 1 1 2 3 4 4 Spartak Moscow 4 1 0 3 6 9 3
KUNDI H CFR Cluj 1 Galatasaray 3 Braga 1 Manchester United 3 Msimamo P W D L F A Pts Manchester United * 4 4 0 0 9 4 12 Galatasaray 4 1 1 2 4 5 4 CFR Cluj 4 1 1 2 5 6 4 Braga 4 1 0 3 5 8 3 * Inaonyesha timu iliyosonga mbele hatua ya mtoano
Zilizochezwa juzi Jumanne KUNDI A Dynamo Kiev 0 Porto 0 Paris St Germain 4 Dinamo Zagreb 0 Msimamo P W D L F A Pts Porto * 4 3 1 0 6 2 10 Paris St Germain 4 3 0 1 10 2 9 Dynamo Kiev 4 1 1 2 5 7 4 Dinamo Zagreb 4 0 0 4 0 10 0 * Inaonyesha timu iliyosonga mbele hatua ya mtoano
Kundi B Schalke 04 2 Arsenal 2 Olympiakos Piraeus 3 Montpellier HSC 1 Msimamo P W D L F A Pts Schalke 04 4 2 2 0 8 5 8 Arsenal 4 2 1 1 7 6 7 Olympiakos Piraeus 4 2 0 2 7 7 6 Montpellier HSC 4 0 1 3 5 9 1
KUNDI C Anderlecht 1 Zenit St Petersburg 0 AC Milan 1 Malaga 1 Msimamo P W D L F A Pts Malaga * 4 3 1 0 8 1 10 AC Milan 4 1 2 1 4 4 5 Anderlecht 4 1 1 2 1 4 4 Zenit St Petersburg 4 1 0 3 3 7 3 * Inaonyesha timu iliyosonga mbele hatua ya mtoano
Kundi D Manchester City 2 Ajax Amsterdam 2 Real Madrid 2 Borussia Dortmund 2 Msimamo P W D L F A Pts Borussia Dortmund 4 2 2 0 6 4 8 Real Madrid 4 2 1 1 10 7 7 Ajax Amsterdam 4 1 1 2 6 8 4 Manchester City 4 0 2 2 6 9 2


No comments:

Post a Comment