Kimenuka... Drogba akilindwa na Polisi wakati akitolewa uwanjani. |
Hatari...! Mashabiki wa 'chama' la kina Drogba wakihaha kujiokoa jana baada ya vurugu kuibuka katika mechi yao dhidi ya Senegal. |
Duh...! Kimenuka hadi kitaa.... mashabiki wa Senegal wakikimbia mitaani huku wakiandamwa na mabomu ya machozi baada ya kuzuka kwa vurugu uwanjani jana. |
Yaya Toure (kulia) na wachezaji wenzake wa Ivory Coast wakitolewa uwanjani na 'FFU' wa Senegal baada ya vurugu zilizotokea uwanjani jana. |
Sasa uwanjani hapakaliki tena...! |
Ni vurugu mtindo mmoja baada ya mashabiki wa Senegal kukasirishwa na kipigo cha Ivory Coast dhidi ya timu yao jana. |
Wachezaji Ivory Coast wakitolewa uwanjani. |
Mashabiki wa Ivory Coast wakihaha kujiweka pamoja ili kujiokoa jana. |
Kimenuka mwanaa... hapakaliki tena uwanjani! |
Kolo Toure (kushoto) akiosha mpira mbele ya nahodha wa Senegal, Pappis Demba Cisse wakati wa mechi hiyo |
Yaya Toure akiwania mpira katikati ya wachezaji wa Senegal |
DAKAR, Senegal
Mechi muhimu ya
kuwania kufuzu kwa fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika kati ya Senegal na Ivory Coast imefutwa baada ya mashabiki
kuvamia uwanja mjini Dakar juzi.
Mashabiki wa wenyeji
walianza kwa kuwasha moto majukwaani na kurusha mawe na vitu vingine uwanjani
wakati Senegal wakiwa nyuma kwa mabao 2-0, matokeo ambayo yangewatoa katika
michuano hiyo.
Mashabiki wa Ivory
Coast walikimbilia uwanjani kuepuka mashambulizi.
Mashabiki na
wachezaji wa Ivory Coast baadaye walitolewa nje na polisi, ambao walifyatua
mabomu ya machozi kuelekea kwenye majukwaa yaliyofurika mashabiki.
Taarifa zimesema kuwa
takriban watu 10 -- akiwamo Waziri wa Michezo wa Senegal, Hadji Malick Gakou --
walijeruhiwa katika vurugu hizo kwenye Uwanja wa Leopold Sedar Senghor.
Vurugu hizo zilitokea
baada ya mshambuliaji wa Ivory Coast, Didier Drogba kufunga goli lake la pili
kwa njia ya penati, huku zikiwa zimebaki dakika 15 kabla mechi kumalizika. Kabla ya goli hilo la penati lililokuwa la 58 kwake kuifungia Ivory Coast, Drogba alifunga goli la kwanza katika mechi hiyo kwa njia ya 'fri-kiki'.
Matokeo hayo
yangeiwezesha Ivory Coast kuongoza kwa jumla ya mabao 6-2 baada ya kushinda pia
kwa mabao 4-2 katika mechi yao ya kwanza.
"Vyakula,
vinywaji na chochote kile kilichoweza kurushwa kilirushwa uwanjani, kutoka
katika kona tofauti," Chris Fuglestad, mwanafunzi wa Marekani anayesoma
mjini Dakar, aliiambia BBC.
Shirikisho la Soka la
Afrika (Caf) bado halijatoa taarifa rasmi kuhusiana na tukiuo hilo. Lakini
afisa mmoja wa Senegal alikaririwa akisema kwamba sasa timu yao itafungiwa na
Caf.
Wachezaji ndugu wa
Manchester City, Yaya na Kolo Toure walikuwamo katika kikosi cha Ivory Coast,
na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya England ilisema katika taarifa yake kuwa:
"Yaya na Kolo Toure wote wako salama baada ya vurugu za mashabiki kuvunja
mechi wakati Senegal walipoikaribisha Ivory Coast mjini Dakar."
Vurugu hizo mjini Dakar zilifunika kufuzu kwa Ghana, Mali, Morocco, Nigeria, Tunisia na mabingwa watetezi Zambia ambao wote wametinga katika fainali hizo zitakazofanyika nchini ya Afrika Kusini Januari mwakani.
Inatarajiwa kuwa Ivory Coast watapewa ushindi lakini hapakuwa na taarifa rasmi kutoka kwenye Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kwa sababu ofisi zao za Cairo zilikuwa zimefungwa.
Vurumai hizo, ambazo zilianika tabia za soka la Afrika, zilipaka tope matukio matamu ya uwanjani katika bara lote huku Zambia wakihitaji ushindi wa "matuta" kufuzu kwenda kutetea taji lao katika fainali hizo za mwakani.
PENALTI ISHIRINI
Ilihitaji penalti 20 kabla ya Wazambia kuifunga Uganda 9-8 baada ya matokeo yao ya jumla kuwa sare ya 1-1 kufuatia kulala 1-0 jijini Kampala.
Tunisia pia walitinga kwenye fainali hizo kwa goli la ugenini baada ya kushikiliwa kwa sare ya 0-0 dhidi ya Sierra Leone nyumbani Monastir, kufuatia sare ya 2-2 katika mechi yao ya awali mwezi uliopita.
Youssef Al Arabi aliifungia Morocco dakika tano kabla ya mechi kumalizika, baada ya kukosa nafasi mbili za awazi, na kulipa taifa lake goli la tatu lililoamua mechi katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Msumbiji mjini Marrakesh ambako walilipa kipigo cha 2-0 walichopata katika mechi yao ya awali.
Lakini mechi hiyo ilizungukwa na utata uliokuja katika dakika ya 60 wakato Morocco walipopewa penalti 'rahisi mno' iliyosababisha nahodha wa Msumbiji, Miro kutolewa kwa kadi nyekundu.
Ghana walikuwa wa kwanza kufuzu baada ya kuifunga Malawi 1-0 ugenini Lilongwe na kupita kwa jumla ya magoli 3-0 shukrani kwa bao la Afriyie Acquah aliyekuwa akiichezea timu ya taifa kwa mara ya kwanza. Mali walitoa kipigo kikali cha 4-1 dhidi ya Botswana na kupita kwa jumla ya magoli 7-1 mjini Lobatse.
Hata hivyo, walifunikwa na kipigo kizito zaidi kilichotolewa na Nigeria dhidi ya Liberia cha magoli 6-1 mjini Calabar ambapo nyota wawili wa Chelsea, Victor Moses aliyepiga mawili na John Obi Mikel 'alitupia' kwa penalti. Nigeria walifunga katika dakika kabla ya kuwang'oa wageni kwa juma la ya mabao 8-3.
Nchi ndogo ya visiwa Cape Verde iliitoa Cameroon ambayo imewahi kucheza robo fainali ya Kombe la Dunia leo na kufuzu kwa mara ya kwanza kucheza fainali za Mataifa ya Afrika licha ya kulala 2-1 katika mechi yao ya marudiano.
Cape Verde yenye wakazi 500,000 ilitoa pigo la kushangaza zaidi katika historia ya michuano hiyo kwa ushindi wa jumla ya magoli 3-2 kufuatia ushindi wao wa nyumbani wa 2-0 mwezi uliopita.
Cape Verde walitarajia kukumbana na kipigo kikali, lakini ilitangulia kupata bao katika dakika ya 22 kupitia 'fri-kiki' ya mshambuliaji anayecheza soka la kulipwa Ureno, Heldon.
Achille Emana alisawazisha dakika chache baadaye lakini walihitaji goli la dakika ya nne ya majeruhi kupata goli lao la pili kupitia kwa mtokea benchi yosso wa miaka 16, Fabrice Olinga kufuatia krosi ya Samuel Eto'o, ambalo halikuwasaidia.
Ukanda wa CECAFA ulipata mwakilishi leo baada ya Ethiopia kushinda nyumbani 2-0 dhidi ya Sudan na kupita kwa magoli ya ugenini baada ya awali kulala 5-3.
Manucho aliifungia Angola magoli mawili katika ushindi wa 2-0 nyumbani dhidi ya Zimbabwe leo na kupita kwa faida ya goli la ugenini baada ya awali kulala 3-1.
Vurugu hizo mjini Dakar zilifunika kufuzu kwa Ghana, Mali, Morocco, Nigeria, Tunisia na mabingwa watetezi Zambia ambao wote wametinga katika fainali hizo zitakazofanyika nchini ya Afrika Kusini Januari mwakani.
Inatarajiwa kuwa Ivory Coast watapewa ushindi lakini hapakuwa na taarifa rasmi kutoka kwenye Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) kwa sababu ofisi zao za Cairo zilikuwa zimefungwa.
Vurumai hizo, ambazo zilianika tabia za soka la Afrika, zilipaka tope matukio matamu ya uwanjani katika bara lote huku Zambia wakihitaji ushindi wa "matuta" kufuzu kwenda kutetea taji lao katika fainali hizo za mwakani.
PENALTI ISHIRINI
Ilihitaji penalti 20 kabla ya Wazambia kuifunga Uganda 9-8 baada ya matokeo yao ya jumla kuwa sare ya 1-1 kufuatia kulala 1-0 jijini Kampala.
Tunisia pia walitinga kwenye fainali hizo kwa goli la ugenini baada ya kushikiliwa kwa sare ya 0-0 dhidi ya Sierra Leone nyumbani Monastir, kufuatia sare ya 2-2 katika mechi yao ya awali mwezi uliopita.
Youssef Al Arabi aliifungia Morocco dakika tano kabla ya mechi kumalizika, baada ya kukosa nafasi mbili za awazi, na kulipa taifa lake goli la tatu lililoamua mechi katika ushindi wa 4-0 dhidi ya Msumbiji mjini Marrakesh ambako walilipa kipigo cha 2-0 walichopata katika mechi yao ya awali.
Lakini mechi hiyo ilizungukwa na utata uliokuja katika dakika ya 60 wakato Morocco walipopewa penalti 'rahisi mno' iliyosababisha nahodha wa Msumbiji, Miro kutolewa kwa kadi nyekundu.
Ghana walikuwa wa kwanza kufuzu baada ya kuifunga Malawi 1-0 ugenini Lilongwe na kupita kwa jumla ya magoli 3-0 shukrani kwa bao la Afriyie Acquah aliyekuwa akiichezea timu ya taifa kwa mara ya kwanza. Mali walitoa kipigo kikali cha 4-1 dhidi ya Botswana na kupita kwa jumla ya magoli 7-1 mjini Lobatse.
Hata hivyo, walifunikwa na kipigo kizito zaidi kilichotolewa na Nigeria dhidi ya Liberia cha magoli 6-1 mjini Calabar ambapo nyota wawili wa Chelsea, Victor Moses aliyepiga mawili na John Obi Mikel 'alitupia' kwa penalti. Nigeria walifunga katika dakika kabla ya kuwang'oa wageni kwa juma la ya mabao 8-3.
Nchi ndogo ya visiwa Cape Verde iliitoa Cameroon ambayo imewahi kucheza robo fainali ya Kombe la Dunia leo na kufuzu kwa mara ya kwanza kucheza fainali za Mataifa ya Afrika licha ya kulala 2-1 katika mechi yao ya marudiano.
Cape Verde yenye wakazi 500,000 ilitoa pigo la kushangaza zaidi katika historia ya michuano hiyo kwa ushindi wa jumla ya magoli 3-2 kufuatia ushindi wao wa nyumbani wa 2-0 mwezi uliopita.
Cape Verde walitarajia kukumbana na kipigo kikali, lakini ilitangulia kupata bao katika dakika ya 22 kupitia 'fri-kiki' ya mshambuliaji anayecheza soka la kulipwa Ureno, Heldon.
Achille Emana alisawazisha dakika chache baadaye lakini walihitaji goli la dakika ya nne ya majeruhi kupata goli lao la pili kupitia kwa mtokea benchi yosso wa miaka 16, Fabrice Olinga kufuatia krosi ya Samuel Eto'o, ambalo halikuwasaidia.
Ukanda wa CECAFA ulipata mwakilishi leo baada ya Ethiopia kushinda nyumbani 2-0 dhidi ya Sudan na kupita kwa magoli ya ugenini baada ya awali kulala 5-3.
Manucho aliifungia Angola magoli mawili katika ushindi wa 2-0 nyumbani dhidi ya Zimbabwe leo na kupita kwa faida ya goli la ugenini baada ya awali kulala 3-1.
No comments:
Post a Comment