Wednesday, October 31, 2012

DIAMOND, RECHO KUTUMBUIZA REDDS MISS TANZANIA... VIINGILIO VYATANGAZWA

Mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu fainali ya shindano la taifa la Redds Miss Tanzania zitakazofanyika Jumamosi kwenye Ukumbi wa Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni katibu mkuu wa kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majaliwa.

Mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu fainali ya shindano la taifa la Redds Miss Tanzania zitakazofanyika Jumamosi kwenye Ukumbi wa Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni katibu mkuu wa kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majaliwa.

Mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu fainali ya shindano la taifa la Redds Miss Tanzania zitakazofanyika Jumamosi kwenye Ukumbi wa Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni katibu mkuu wa kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majaliwa.

Mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga (kulia) akizungumza na waandishi wa habari kuhusu fainali ya shindano la taifa la Redds Miss Tanzania zitakazofanyika Jumamosi kwenye Ukumbi wa Blue Pearl Hotel, Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam. Kushoto kwake ni katibu mkuu wa kamati ya Miss Tanzania, Bosco Majaliwa.

MSANII wa muziki wa kizazi kipya, Diamond Platnumz, Rachel na Wanne Star, ni miongoni wasanii watakaosindikiza fainali za shindano la urembo la Redd's Miss Tanzania 2012 kwenye ukumbi wa Blue Pearl Hotel,  Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam Jumamosi.

Vimwana 30 watachuana katika kuwania kurithi mikoba ya Miss Tanzania wa sasa, Salha Israel.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar Es Salaam leo, mkurugenzi wa kampuni ya Lino Agency, Hashim Lundenga, alisema maandalizi yako katika hatua za mwisho kwa ajili ya kumsaka mwakilishi huyo wa nchi katika fainali za urembo za dunia, Miss World 2013.

Lundenga alisema tiketi kwaajili ya shindano hilo zipo tayari na zipo kwa idadi maalum na leo hii zimeanza kuuzwa katika vituo vilivyopendekezwa kulingana na maoni ya wadau.

"Kutokana na ukubwa wa shindano kwa mwaka huu wale wote watakaofanikiwa kuingia ukumbini watakaa katika viti maalum vilivyowekwa katika hadhi ya kimataifa na kila tiketi itagarimu kiasi cha Sh. laki moja (100,000) za Kitanzania," alisema.

Alisema wanatarajia ushindani mkali hasa kwa kuzingatia kuwa sehemu kubwa ya warembo wao ni wasomi walio katika ngazi ya elimu ya juu nchini.

Alivitaja vituo vilivyoanza kuuza tiketi leo kuwa Stears Samora,
Regency Park Hotel, Rose Garden Mikocheni, Share Illusion-Mlimani City, Giraffe Hotel, Ubungo Plaza na ofisi za Lino na City Sports Lounge iliyopo Posta Mpya mkabala na Mnara wa Askari.

"Nitoe rai kwa wapenzi wote, ni vyema wapate tiketi mapema ili kuepuka usumbufu kwa sababu kuna kikomo cha tiketi kilichopo kama tulivyotangaza awali," alisema Lundenga.

Alisema warembo watano tayari wameingia katika Top 15 baada ya kushinda mataji madogo. Aliwataja kuwa ni Lucy Stephano aliyetwaa taji dogo la Miss Photogenic, Magdalena Roy (Miss Top Model), Mary Chizi (Miss Top Sport Woman), Babylove Kalala (Miss Talent) na Happiness Daniel aliyetwaa taji la Miss Personality baada ya kupigiwa kura na warembo wenzake.

"Mwisho napenda kutoa shukrani zangu kwa wadhamini wetu ambao ni TBL kupitia kinywaji chao cha Redds Original, Star TV na Giraffe Hotel," alisema Lundenga.     

Mshindi wa taji la mwaka huu atapewa gari, ambalo litatambulishwa siku ya onyesho na fedha taslimu Sh. milioni 8.

No comments:

Post a Comment