Saturday, October 27, 2012

BABYLOVE KALALA AWA WA TATU KUTINGA TOP 15 REDD'S MISS TANZANIA... ACHEZEA CHATU NA KUTWAA TAJI LA MREMBO MWENYE KIPAJI

Mshindi wa Redd's Miss Talent 2012, Babylove Kalala akionyesha umahiri wake wa kuchezea nyoka aina ya chatu uliompa ushindi wa taji la Miss Talent
Mshindi wa Redd's Miss Talent 2012, Babylove Kalala (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na warembo wengine walioingia hatua ya tano bora ya Redd's Miss Talent iliyofanyika kwenye hoteli ya Giraffe jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo. Kutoka kulia ni mshiriki namba 13 kutoka kanda ya Mashariki, Joyce Baluhi, mshiriki namba 15 kutoka Temeke, Catherine Masumbigana, mshiriki kutoka Kanda ya Mashariki, Irene Verda na mshiriki namba 26 kutoka Kinondoni, Brigit Alfred.
Mshindi wa Redd's Miss Talent 2012, Babylove Kalala (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na warembo wengine walioingia hatua ya tano bora ya Redd's Miss Talent iliyofanyika kwenye hoteli ya Giraffe jijini Dar es Salaam usiku wa kuamkia leo. Kutoka kulia ni mshiriki namba 13 kutoka kanda ya Mashariki, Joyce Baluhi, mshiriki namba 15 kutoka Temeke, Catherine Masumbigana, mshiriki kutoka Kanda ya Mashariki, Irene Verda na mshiriki namba 26 kutoka Kinondoni, Brigit Alfred.

Mshiriki namba 16 kutoka Kanda ya Mashariki, Irene Verda akionyesha umahiri wake wa kupuliza saxophone.
Mh! Huyu kazoea kushika haya manyoka... Babylove Kalala akionyesha ujasiri wa kuchezea nyoka wakati mrembo huyo na wenzake wanaowania taji hilo walipotembelea eneo la Snake Park, Arusha kujionea nyoka wa aina mbalimbali, mamba, kenge, ndege aina ya bundi, tai na tumbili katika ziara ya kuhamasisha utalii wa ndani
Babylove Kalala akionyesha ujasiri wa kumuuma wakati mrembo huyo na wenzake wanaowania taji hilo walipotembelea eneo la Snake Park mjini Arusha.

Na Mwandishi wetu
MREMBO kutoka Kagera anayewakilisha Kanda ya Ziwa katika shindano la Redd’s Miss Tanzania, Babylove Kalala juzi usiku alitwaa taji la Redd’s Miss Talent lililofanyika kwenye hoteli ya Giraffe, iliyopo Kunduchi, Dar es Salaam.

Kutokana na ushindi huo, Babylove sasa anaungana na Miss Photogenic, Lucy Stephano na Redd's Miss Tanzania Sports Lady, Mary Chizi kuingia hatua ya 15-Bora ya fainali ya Redd’s Miss Tanzania itakayofanyika mwishoni mwa wiki.

Babylove aliwashinda warembo wengine 29 aliokuwa anachuana nao baada ya kuonesha kipaji cha hali ya juu wakati akicheza ngoma kwa kutumia nyoka, kiumbe ambaye warembo wengine walionekana kumuogopa mno.

Warembo wengine walioingia hatua ya 5-Bora ya Miss Talent walikuwa ni Joyce Baluhi na Irene Verda wa Kanda ya Mashariki, Catherine Masumbigana (Temeke) na Brigit Alfred (Kinondoni).

Mgeni rasmi katika shindano hilo alikuwa Mbunge wa Viti Maalum (CCM), Catherine Magige ambaye aliwataka warembo wanaoshiriki kutumia mashindano hayo kama chachu ya kufikia malengo waliyojiwekea.

Akizungumza mara baada ya kutwaa taji hilo, Babylove aliwashukuru washiriki wengine kwa kuwa chachu ya yeye kuhakikisha anakuwa mbunifu zaidi, huku akiahidi kufanya makubwa katika shindano la Redd’s Miss Tanzania.

Shindano la Redd’s Miss Tanzania kwa sasa linadhaminiwa na kinywaji cha Redd’s Original kinachozalishwa na Kampuni ya Bia Tanzania (TBL).

No comments:

Post a Comment