Sunday, September 9, 2012

VITALI KLITSCHKO AMMWAGA DAMU MANUEL CHARR MWILI MZIMA KATIKA TKO RAUNDI YA NNE

Bingwa wa dunia wa ngumi za uzito wa juu wa taji la WBC, Vitali Klitschko (kulia) akiendelea kumsukumia mangumi mpinzani wake Mjerumani Manuel Charr aliyetapakaa damu mwili mzima wakati wa raundi ya nne ya pambano lao mjini Moscow jana usiku Septemba 8, 2012.
Bingwa wa dunia wa ngumi za uzito wa juu wa taji la WBC, Vitali Klitschko (kulia) akimchapa mpinzani wake Mjerumani Manuel Charr wakati wa pambano lao mjini Moscow jana usiku Septemba 8, 2012.

Bingwa wa dunia wa ngumi za uzito wa juu wa taji la WBC, Vitali Klitschko (kulia) akimchapa mpinzani wake Mjerumani Manuel Charr wakati wa pambano lao mjini Moscow jana usiku Septemba 8, 2012.

Mjerumani Manuel Charr akijibu mapigo dhidi ya bingwa wa dunia wa ngumi za uzito wa juu wa taji la WBC, Vitali Klitschko (kulia) wakati wa pambano lao mjini Moscow jana usiku Septemba 8, 2012.

Mjerumani Manuel Charr (wa pili kushoto) akipinga baada ya refa kusimamisha pambano lake dhidi ya Vitali Klitschko. Kabla ya kipigo cha jana, Charr alikuwa amepigana mara 20 na kushinda yote.

Mjerumani Manuel Charr (wa pili kushoto) akipinga baada ya refa kusimamisha pambano lake dhidi ya Vitali Klitschko na kumaanisha kwamba amepigwa kwa TKO, likiwa ni pambano lake la kwanza kupigwa. Kabla ya kipigo cha jana, Charr alikuwa amepigana mara 20 na kushinda yote.

Charr akiwa ametapakaa damu huku akiendelea kumuwinda mpinzani wake Vitali baada ya kuchanwa chini ya jicho lake la kulia. Charr alikuja juu baada ya pambano hilo kusimamishwa akilalamikia kitendo cha kuchanwa chini ya jicho akiashiria kuwa si ngumi iliyomkata bali pengine kamba za gloves. Alipiga mateke kamba za ulingo kuonyesha fadhaa yake na akapanda katika kamba za kila kona ya ulingo na kunyanyua mikono juu kama mtu aliyeshinda huku akishangiliwa na baadhi ya mashabiki wa nyumbani.

Manuel Charr 'akilamba sakafu' katika raundi ya pili ya pambano lake aliloelemewa mno chini ya bingwa mtete wa taji la WBC la ndondi za uzito wa juu usiku wa kuamkia leo

Charr akiwa ametapakaa damu huku akiendelea kubadilishana masumbwi na mpinzani wake Vitali baada ya kuchanwa chini ya jicho lake la kulia. Charr alikuja juu baada ya pambano hilo kusimamishwa akilalamikia kitendo cha kuchanwa chini ya jicho akiashiria kuwa si ngumi iliyomkata bali pengine kamba za gloves. Alipiga mateke kamba za ulingo kuonyesha fadhaa yake na akapanda katika kamba za kila kona ya ulingo na kunyanyua mikono juu kama mtu aliyeshinda huku akishangiliwa na baadhi ya mashabiki wa nyumbani.

Baada ya hasira kupoa, Charr alirejea katika uungwana wa michezo na kumpa mkono mshindi Vitali Klitschko

Vitali Klitschko (kushoto) akitangazwa mshindi na refa Guido Cavalleri baada ya kumpiga Manuel Charr (kulia) wakati wa pambano lao la ndondi la uzito wa juu la kuwania taji la WBC mjini Moscow usiku wa kuamkia leo. Klitschko alitetea taji lake baada ya refa kusimamisha pambano katika raundi ya nne. Picha: REUTERS

Vitali Klitschko akishangilia baada ya kutangazwa mshindi dhidi ya Manuel Charr wakati wa pambano lao la ndondi la uzito wa juu la kuwania taji la WBC mjini Moscow usiku wa kuamkia leo. Klitschko alitetea taji lake baada ya refa kusimamisha pambano katika raundi ya nne. Picha: REUTERS
Vitali Klitschko akishangilia kwa kubeba bendera ya nchi yake ya Ukraine baada ya kutetea kimafanikio taji lake la ndondi la uzito wa juu la kuwania taji la WBC baada ya kumpiga Manuel Charr mjini Moscow usiku wa kuamkia leo. Picha: REUTERS
Nimekubali we mkali.... hapa hasira zimeisha.  Manuel Charr (kushoto) akimpongeza Vitali Klitschko baada ya pambano lao

BINGWA wa dunia wa ndondi za uzito wa juu wa WBC, Vitali Klitschko alimsambaratisha mapema mpinzani wake Mjerumani Manuel Charr, kwa TKO ya raundi ya nne mjini Moscow.

Klitschko (41) alipata ushindani mdogo mno kutoka kwa mpinzani wake huyo ambaye hapo kabla alikuwa hajawahi kupoteza pambano.

Bondia huyo wa Ukraine alimlambisha sakafu mzaliwa wa Beirut, Charr (27) kwa ngumi kali ya mkono wa kulia katika raundi ya pili.

Na Charr, ambaye ushindi wake unaokumbukwa zaidi ni dhidi ya Muingereza Danny Williams, alisimamishwa katika raundi ya nne kutokana na damu kumwagika kama maji kutoka chini ya jeraha alilopata chini ya jicho lake la kulia.

Alicharuka kwa hasira kufuatia maamuzi hayo - yaliyotokana na madaktari waliokagua jeraha hiyo - na akapinga matokeo kwa muda wote bila ya mafanikio.

Pambano la Klitschko lilikuwa ni la ushindi wa pointi dhidi ya Muingereza Dereck Chisora mwezi Februari, lakini mechi hiyo ilifunikwa na tukio la mkazi huyo wa London dhidi ya Muingereza mwenzake David Haye kuishia kutaka kuzipiga katika vurugu kubwa iliyozuka wakati wa mkutano na wana habari baada ya pambano.

Haye, ambaye alipigwa kwa pointi na mdogo wake Klitschko, Wladimir mwaka jana, alikuja kumpiga Chisora kwa KO Julai na tangu wakati huo amekuwa akisukuma mambo akitaka apigane na Vitali.

Kutokea kwa pambano hilo kutatarajia kama Klitschko hatastaafu na kuweka nguvu zake katika siasa.

Rekodi zao


Klitschko Charr
45 Kushinda 21
0 Sare 0
2 Kupigwa 1
41 KO 11
41 Umri 27
6ft 7in Urefu 6ft 3½in
79in Urefu wa mkono 77in

No comments:

Post a Comment