Friday, September 7, 2012

RVP NIMEBARIKIWA KUCHEZA CHINI YA WENGER NA FERGIE

Straika wa Manchester United, Robin van Persie
Van Persie akimkumbatia kocha Arsene Wenger baada ya "kutupia" wakati akiichezea Arsenal.


Van Persie akimkumbatia SAF katika mazoezi ya klabu yake mpya ya Manchester United
Arsene Wenger (kushoto) na Alex Ferguson (kulia) wakiwa na rais wa UEFA, Michel Platini katika kongamano

STRAIKA wa Manchester United, Robin van Persie amesema ni jambo la kipekee kuwa mmoja wa wachezaji WAWILI tu waliobahatika kucheza chini ya kocha Sir Alex Ferguson na Arsene Wenger.

Kutokana na uhasama uliopo baina ya Manchester United na Arsenal kwa miaka mingi, straika wa Uholanzi, Van Persie anakuwa mchezaji wa pili tu baada ya beki Mfaransa Mikael Silvestre kucheza chini ya makocha hao wawili.

"Nimekuwa chini ya makocha 'spesho'," aliiambia OnsOranje, tovuti rasmi ya mashabiki ya chama cha soka cha Uholanzi.

"(Bert) van Marwijk, Wenger, (Marco) van Basten, Ferguson. Piece hawa ni makocha 'spesho' kabisa.

"Nadhani nimekuwa mmoja wa wachezaji wachache ambao wamepata kucheza chini ya Wenger na Ferguson. Hilo ni jambo la kipekee."

No comments:

Post a Comment