Monday, September 3, 2012

RONALDO AMWAMBIA RAIS REAL MADRID ANATAKA KUONDOKA

Straika wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akigugumia kwa maumivu baada ya kuchezewa rafu wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Granada kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Septemba 2, 2012. Ronaldo alitolewa kufuatia rafu hiyo. Real walishinda 3-0. Picha: REUTERS
Kiungo wa Real Madrid, Luka Modric (kulia) akiwania mpira dhidi ya mchezaji wa Granada, Inigo Lopez wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya Hispania kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Septemba 2, 2012. Real walishinda 3-0. Picha: REUTERS

Straika wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akigugumia kwa maumivu baada ya kuchezewa rafu wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Granada kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Septemba 2, 2012. Ronaldo alitolewa kufuatia rafu hiyo. Real walishinda 3-0. Picha: REUTERS
Straika wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo (katikati) akipiga shuti wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Granada kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Septemba 2, 2012. Real walishinda 3-0. Picha: REUTERS

Kiungo wa Real Madrid, Sami Khedira akimiliki mpira wakati wa mechi yao ya Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Granada kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Septemba 2, 2012. Real walishinda 3-0. Picha: REUTERS

CRISTIANO Ronaldo amemweleza rais wa Real Madrid, Florentino Perez kwamba anataka KUONDOKA, imebainishwa.

Radio Cadena COPE imesema Ronaldo alikutana na Florentino Jumamoso usiku na kumfahamisha kwamba hana furaha na anataka kuuzwa.

Jana, licha ya kufunga mara mbili katika ushindi wa 3-0 didi ya Granada, Ronaldo alichafua sherehe kwa kutangaza kwamba "hakuwa na furaha" na kwamba jambo hilo linatokana na matatizo katika weledi wa kazi yake - na si maisha yake binafsi.

Ilidaiwa kwamba straika huyo wa zamani wa Manchester United ametofautiana na nyota wengi wa klabu hiyo katika chumba cha kuvalia, wakiwamo Marcelo na Fabio Coentrao.

Hata hivyo, imedaiwa pia kwamba Ronaldo anaona kwamba anahitaji mwanzo mpya kufikia malengo yake na kwamba alifadhaishwa na tukio la kutoswa na UEFA kwa kumtaja kiungo wa Barcelona, Andres Iniesta, kuwa Mwanasoka Bora wa Mwaka wa UEFA.

No comments:

Post a Comment