Wednesday, September 26, 2012

REDDS MISS TANZANIA KUFANYIKA NOV.3 UBUNGO PLAZA

Miss Tanzania 2012, Salha Israel (kushoto) akipita jukwaani na warembo wenzake wakati wa shindano la Miss World nchini China mwaka jana. Mrithi wa Salha atapatikana Nov.3.

Salha (mwenye njano) akiwa na wenzake wakati wa kambi ya shindano la Miss World nchini China mwaka jana.

Salha (wa pili kulia) akiwa na wenzake wakati wa kambi ya shindano la Miss World nchini China mwaka jana.

Salha Israel (wa pili kushoto) akifurahia zawadi yake ya gari aina ya Jeep wakati akikabidhiwa mwaka jana chini ya wadhamini wa waliopita kampuni ya huduma za simu ya Vodacom. Shindano hilo sasa linadhaminiwa na bia ya Redds.

Salha Israel akiwa katika bango la Redds Miss Tanzania 2012 wakati wa uzinduzi wa shindano la mwaka huu

Salha akipita jukwaani wakati shindano la Miss World nchini China mwaka jana.

Salha akipita jukwaani wakati shindano la Miss World nchini China mwaka jana.

Salha Israel akiwa katika bango la Redds Miss Tanzania 2012 wakati wa uzinduzi wa shindano la mwaka huu

Meneja wa bia ya Redd's, Victoria Kimaro (kushoto), alipokuwa akizungumza kuhusu uzinduzi wa msimu mpya wa mashindano ya urembo nchini katika mkutano na wanahabari jijini Dar es Salaam. Kulia ni Miss Tanzania 2011, Salha Israel.
Salha Israel (kulia) akifurahia zawadi yake ya gari aina ya Jeep wakati akikabidhiwa mwaka jana chini ya wadhamini wa waliopita kampuni ya huduma za simu ya Vodacom. Shindano hilo sasa linadhaminiwa na bia ya Redds.
Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga (katikati) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Wengine kushoto ni Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro na kulia ni Miss Tanzania 2012, Salha Israel.

Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro, Miss Tanzania 2012, Salha Israel na mshindi wa nne wa Miss Tanzania 2012, Jennifer Kakolaki.

Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga (wa pili kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Wengine kutoka kushoto ni Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro, Miss Tanzania 2012, Salha Israel na mshindi wa nne wa Miss Tanzania 2012, Jennifer Kakolaki.

Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Wengine ni Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga (katikati) na Miss Tanzania 2012, Salha Israel.

Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Kulia ni Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga.

Mkuu wa Itifaki wa Miss Tanzania, Albert Makoye (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Kulia ni Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro.

Meneja wa Bia ya Redds, Victoria Kimaro (kushoto) akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo kuhusu kambi ya Redd's Miss Tanzania 2012. Wengine ni Mratibu wa mashindano ya  Miss Tanzania, Hashim Lundenga (katikati) na Miss Tanzania 2012, Salha Israel.

SHINDANO la Redds Miss Tanzania 2012 litafanyika Novemba 3 kwenye ukumbi wa Ubungo Plaza jijini Dar es Salaam, waandaaji kamati wa Miss Tanzania wametangaza leo.

Akizungumza na waandishi wa habari kwenye ukumbi wa Idara ya Habari (MAELEZO) jijini Dar es Salaam, mratibu wa shindano hilo, Hashim Lundenga, amesema warembo wataingia kambini Oktoba 2 katika hoteli ya Giraffe, ambako watakaa hadi siku ya shindano.
  
Mshindi wa shindano hilo atamrithi, Salha Israel kutoka Ilala anayeshikilia taji la taifa. Kwa kushinda shindano hilo mwaka jana, Salha alizawadiwa gari kali aina ya Jeep.

Hata hivyo, mapema mwaka huu kamati hiyo iliendesha shindano dogo na kumpata Lissa Jensen ambaye aliwakilisha nchi katika fainali za Dunia kutokana na mabadiliko ya kalenda yaliyofanywa na Kamati ya Miss World.

Miss Tanzania atakayepatikana Novemba 3 atakuwa na muda mrefu wa kujiandaa na atashiriki katika shindano la Miss World la mwakani na utaratibu huo utakuwa wa kudumu.

Hadi sasa, Miss Tanzania aliyepata mafanikio katika shindano hilo la dunia ni Nancy Sumary ambaye alitwaa taji la Miss World Africa 2005.

No comments:

Post a Comment