Wednesday, September 19, 2012

RAIS KIKWETE KWENDA NYUMBANI KWA TUNDU LISSU KESHO... NI KUSHIRIKI TUKIO LA KUAGA MWILI WA BABA YAKE TUNDU LISSU ALIYEFARIKI JUMAPILI


Mhe. Rais Kikwete (kulia) akiwa na Mhe. Tundu Lissu

Mhe. Tundu Lissu (kulia) akiwa na Spika wa Bunge, Mhe. Anna Makinda.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete, ni miongoni mwa viongozi wa juu serikalini watakaoshiriki  tukio la kuuaga mwili wa baba wa Mbunge wa Singida Mashariki (CHADEMA), Mhe. Tundu Lissu, aliyefariki dunia Jumapili kwenye Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Akizungumza leo, Mhe. Tundu Lissu amesema kuwa shughuli za kumuaga marehemu baba yake zitafanyika kesho kuanzia asubuhi nyumbani kwake (Mhe. Tundu Lissu), eneo la Tegeta jijini Dar es Salaam na kwamba, wamejulishwa kuwa Rais Kikwete ni miongoni mwa viongozi watakaohudhuria.     

Akieleza zaidi, Mhe. Lissu amesema kuwa ratiba ya tukio hilo itaanza saa 5:00 asubuhi, misa ya marehemu itaanza saa 7:00 mchana na baada ya hapo, litafuatia tukio la kusoma wasifu na na kutoa heshima za mwisho kwa marehemu kabla ya kuanza safari ya kwenda kuzika nyumbani kwao Mahambe, katika wilaya mpya ya Ikungi mkoani Singida.

"Mzee amefariki akiwa na miaka 86. Tumejaribu sana kumtibu, Mungu ndiye anayejua zaidi... tunashukuru sana kwa ushirikiano mkubwa tunaopata kutoka kwa ndugu na jamaa," amesema Mhe. Tundu Lissu leo wakati akihojiwa na mtandgazaji Anord Kayanda wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa jioni na kituo cha redio cha Clouds FM.



No comments:

Post a Comment