Thursday, September 13, 2012

INIESTA AJERUHIWA… KUKOSA MECHI TATU BARCELONA


Andres Iniesta
BARCELONA, Hispania
Andres Iniesta na Jordi Alba walirejea kutoka katika majukumu ya kuichezea timu ya taifa lao wakiwa na majeraha na maradhi licha ya kwamba wote walicheza kwa dakika zote 90 wakati wakiisaidia Hispania kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya Georgia Jumanne usiku.
Iniesta aliumia msuli wa katikati ya goti na paja la mguu wa kulia na madaktari wa Barcelona wamethibitisha kuwa atakuwa nje kwa siku 10-15.

Kiungo huyo hatakuwamo katika kikosi cha timu yake kitakachocheza keshokutwa Jumamosi mechi ya ugenini ya La Liga, Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Getafe na ya nyumbani dhidi ya Granada. Atakosa pia mechi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kati ya Barcelona na Spartak Moscow itakayopigwa Jumatano.

Jordi Alba yuko shakani pia kucheza keshokutwa dhidi ya Getafe, lakini hajaondolewa katika kikosi kitakachokuwa Madrid kucheza mechi hiyo.

No comments:

Post a Comment