Thursday, September 27, 2012

BAYERN MUNICH WAMTOLEA MACHO THEO WALCOTT... WATAKA KUMNG'OA ARSENAL AMRITHI FRANCK RIBERY

Theo Walcott
Bayern Munich wanafuatilia mchakato wa kusainiwa kwa mkataba mpya wa winga wa Arsenal, Theo Walcott kwa nia ya kumnyakua ikibidi ili akarithi nafasi ya winga wao Franck Ribery anayefukuziwa na klabu ya nchini kwao Ufaransa ya matajiri wa PSG.

Walcott atakuwa huru kusaini mkataba wa makubaliano ya awali na klabu nyingine kufikia Januari 1 na kocha Arsene Wenger amekiri kwamba wanaweza kumuuza kama atakataa kusaini mkataba  mpya waliompa kabla ya krismasi.

Gazeti la TZ limesema kuwa Bayern wanafuatilia kwa karibu maendeleo ya kusainiwa kwa mkataba mpya wa Walcott.

No comments:

Post a Comment