Saturday, August 18, 2012

WENGER: TUWE WAKWELI JAMANI... ARSENAL TUSINGEWEZA KUSHINDANA NA MAN U KWA KUMLIPA VAN PERSIE MSHAHARA WA MILIONI 615/- KWA WIKI....!

Kijana hapa utakuwa bilionea kwa mihela tunayokupa kila wiki na pia kabati lako litajaa makombe kwa sababu sisi ni watu wa kazi... ila lazima ukaze msuli, ukilegea nakuchenjia kama Berbatov! Kocha Alex Ferguson akimpa maelekezo straika wake mpya, Robin van Persie wakati wakiwa mazoezini jijini Manchester jana. 
Huyu Ferguson haniwezi kwa lolote.... ila kinachombeba ni kumwaga mapesa tu! Kocha Arsene Wenger wa Arsenal (kushoto) akiwa na Alex Ferguson. 
Asante sana kwa kuniachia hili jembe Van Persie... Ferguson (kulia) akiwa na Wenger
LONDON, England
Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema leo kwamba klabu yao haikuweza kushindana na mkataba wa Manchester United uliombatana na mshahara mnono kwa straika na nahodha wao wa zamani, Robin van Persie.

Amesema: “Sisi tunaishi kwa kuzingatia hali halisi kiuchumi lakini klabu nyingine hazizingatii jambo hilo. Kuna baadhi ya vitu hatuwezi kamwe kuvifanya.

“Mnataka kulipa kiasi gani? 250k (Sh. milioni 615)?, 300k (Sh. milioni 740)? Mnasema sisi hatuishi kulingana na uhalisia uliopo duniani halafu bado mnatuhoji tunaposema kwamba hatutalipa mshahara wa 250k (Sh. milioni 615) kwa wiki.”

Wenger pia alifichua kwamba Arsenal hawatawekeza zaidi fedha walizopata kwa kumuuza Van Persie paundi za England milioni 22 (Sh. bilioni 55) kwani tayari wameshawasajili mastraika Lukas Podolski, Olivier Giroud na kiungo Santi Cazorla.

Arsenal walimuuza Van Persie kwa paundi za England milioni 24 (Sh. bilioni 60), huku paundi milioni 22 kati ya fedha hizo zikilipwa taslim na nyingine zikitarajiwa kutolewa ikiwa straika huyo ataonyesha kiwango kizuri na kuipa mafanikio klabu yake mpya ya Man U.     

No comments:

Post a Comment