Saturday, August 18, 2012

JINI KABULA: NINA UJAUZITO WA BUSHOKE

Miriam Jolwa a.k.a Jini Kabula
Jini Kabula

MSANII wa filamu nchini, Miriam Jolwa maarufu kama 'Jini Kabula' amesema anajiandaa kupata mtoto wake wa pili kwani tayari ana ujauzito wa msanii Bushoke.

"Nimempenda anajua mambo ndio maana nimebeba ujauzito wake," alisema kimwana huyo wakati akihojiwa na mtangazaji Sam Misago a.k.a Presenters' Prezident katika kipindi cha Friday Night Live cha EATV jana usiku. 

"Napenda watoto, ukiwazaa unakuwa mtamu zaidi... ukitoa mimba unakomaa. Nitawazaa wote hata kama nina mayai 100, nitawazaa wote.

"Mimi siwezi kutoa mimba. Kama mama yangu angenitoa nisingekuwepo leo hii."

Sam Misago akamuuliza: "Kama unasema Bushoke anajua mambo, Mr Chuzi je?"

Kabula akajibu: "Siwezi kumkana. Ni baba wa mtoto wangu wa kwanza. Naye anajua mambo ndio maana nikamzalia."

Jini  Kabula (kushoto) akiwa na Mr Nice.

Sam akampiga swali jingine: "Na Mr Nice je, mbona hukumzalia?"

Kabula akajibu: "Ah! Mir Nice sikumpenda. We unadhani unamzalia kila mtu? Wengine hawajui matunzo ya watoto wao."

Alipoulizwa hahofii kukimbiwa na mwanaume aliyembebea ujauzito, Kabula alisema hahofii jambo hilo kwa sababu yeye ana kipato cha kutosha kumfanya mwanae aishi maisha mazuri.

Alipoulizwa ni nani kati yake na Bushoke aliyehitaji mtoto huyo, Kabula alisema: "Bushoke ndiye aliyeng'ang'ania kuzaa na mimi, alitaka hii mbegu, huoni mi' ni mtoto mkali?"

Jini Kabula alifika katika studio ya EATV kwa ajili ya kupromoti video ya wimbo wa kundi lao jipya la muziki la vimwana watatu la Scorpion Queens. Wengine katika kundi hilo mshiriki wa zamani wa Miss Tanzania, Rashida Wanjara na Isabella Mpanda.

"Hatujavamia fani ya muziki, mimi nilipenda muziki tangu sijawaza kwamba nitakuwa kuwa nyota wa Bongo Movies," alisema Kabula.

Kuhusu sababu ya kujiita Scorpion, Kabula alisema: "Sisi tuna sifa za ng'e, unaweza ukaishi naye hata ndani ya nyumba kama hutamchokoza, lakini ukimkanyaga utakiona cha moto."

Aidha, Kabula alisema video ya wimbo wao mpya imewagharimu Sh. milioni 9.1 na kwamba huo ni mwanzo tu kwani wanajipanga kutoa wimbo wao wa pili kabla ya mwisho wa mwaka huu.


Kwenye kipindi hicho cha Friday Night Live, alikuwapo pia muigizaji Sinta, ambaye alikutana na boifrendi wake wa zamani Juma Nature, ambaye amecheza naye filamu itakayotoka hivi karibuni ya 'Sitaki Demu', wimbo wa Nature ambao aliutunga kumshambulia Sinta wakati walipoachana huku akimpenda mno.

No comments:

Post a Comment