Thursday, August 9, 2012

RONALDO AJIPA MOYO TUZO MWANASOKA BORA WA DUNIA

Cristiano Ronaldo
NEW YORK, Marekani
Cristiano Ronaldo amekuwa akishinda tuzo nyingi akiwa na Real Madrid hadi kufikia mwaka huu 2012, lakini amekiri kwamba kuna tuzo moja tu ambayo anataka kuiona kufikia mwishoni mwa mwaka huu.

Nayo ni tuzo nyingine ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia (FIFA Ballon d'Or).
"Itakuwa safi sana (kuwa mshindi wa tuzo hiyo)," Ronaldo amesema leo.


Straika huyo amekiri kwamba mwanzoni mwa msimu uliopita alipania kutwaa tuzo nyingi kadri itakavyowezekana kwa ajili ya klabu yake ya Real Madrid na yeye mwenyewe. Hadi sasa mambo si mabaya sana kwa nyota huyo wa Ureno, aliyeiongoza klabu yake kutwaa ubingwa wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania na pia kuibuka kinara kati ya wacheaji 50 waliokuwa wakiwania Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa mtandao wa habari za soka wa Goal.com (Goal.com 50).

Lakini, baada ya kupoteza tuzo ya Ballon d'Or kwa straika wa  Barcelona, Lionel Messi katika miaka mitatu iliyopita, Ronaldo sasa ana matarajio makubwa ya kutunukiwa tuzo hiyo yenye hadi kubwa zaidi duniani.

"Itakuwa na maana kubwa sana kwangu, nimejituma sana katika msimu wote uliopita ili kutwaa tuzo za pamoja na zangu binafsi," alisema.

Real Madrid hivi sasa iko katika ziara ya maandalizi ya msimu nchini Marekani ambako inacheza mechi kadhaa za kirafiki. Hadi sasa imeshacheza mechi tatu na kushinda zote dhidi ya LA Galaxy, Santos Laguna na AC Milan.

Baada ya kufunga mabao mawili jana na kuisaidia Real kuibuka na ushindi wa 5-1 dhidi ya Milan, kwenye Uwanja wa Yankee, Ronaldo alitajwa kuwa ndiye Mchezaji Bora wa Mechi.

Straika huyo alishangiliwa na maelfu ya mashabiki waliojazana uwanjani kila mara alipogusa mpira na alionekana kufurahia sana tuzo ya kuwa mcheaji bora wa mechi.

Ronaldo alishinda tuzo yake ya kwanza ya FIFA Ballon d'Or mwaka 2008 baada ya kuisaidia Manchester Untied kutwaa makombe mawili kwa mpigo, wakibeba taji la Ligi Kuu ya England na Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.


No comments:

Post a Comment