Thursday, August 9, 2012

MANCHESTER UNITED HATIMAYE YATUMA MAOMBI RASMI ARSENAL YA KUMSAJILI ROBIN VAN PERSIE


Straika Van Persie
LONDON, England
MANCHESTER United wanajaribu kumsajili straika wa kimataifa wa Uholanzi, Robin Van Persie kutoka kwa mahasimu wao katika Ligi Kuu ya England, klabu ya Arsenal, amesema leo kocha Alex Ferguson.

"Tayari tumetuma maombi yetu," Ferguson ameiambia tovuti ya klabu yake (www.manutd.com).

"Tunajitahidi kumpata kadri inavyowezekana, lakini hadi kufikia wakati huu bado hatujapiga hatua.

"Hatutaki kuwasemea Arsenal. Sijui wanafikiria nini kwa sababu hawajatujibu chochote."

Van Persie alitangaza mwezi uliopita kwamba hataongeza mkataba wa kuendelea kuichezea Arsenal kwa sababu hakuwa akifurahishwa na mwelekeo wa klabu hiyo.

Straika huyo mwenye miaka 29, ambaye amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake, amekuwa na klabu ya Arsenal tangu mwaka 2004.

Van Persie alikuwa ndiye mfungaji bora wa msimu uliopita katika Ligi Kuu ya England baada ya kufikisha mabao 30, matatu zaidi ya straika wa Man U, Wayne Rooney aliyemfuatia katika nafasi ya pili.

Msimu mpya utaanza Agosti 18.

No comments:

Post a Comment