Thursday, August 9, 2012

MAN U WAKUBALI KUMLIPA ROBIN VAN PERSIE MSHAHARA WA KILA WIKI WA MILIONI 530/-

Van Persie akiwa mazoezini jana katika kambi ya Arsenal iliyopo Ujerumani kujiandaa na msimu mpya.  
LONDON, England
Man U wamekubali kumlipa straika Robin van Persie mshahara unolingana na Wayne Rooney ili kumsajili nahodha huyo wa mahasimu wao katika Ligi Kuu ya England, klabu ya Arsenal.

Gazeti la The Telegraph limesema leo kwamba utayari wa Man U kumlipa Van Persie mshahara wa wiki wa paundi za England 220,000 (Sh. milioni 533) kama anaoupata Rooney umetokana na nia yao ya kuhakikisha kwamba wawili hao wanakuwa na umuhimu unalingana.

Imeelezwa kuwa 'ofa' ya msharahara mnono kwa straika huyo wa kimataifa wa Uholanzi ambaye hivi sasa ana miaka 29, inaweza kumchanganya  Van Persie na kumuongezea kasi katika kutimiza dhamira yake ya kuondoka Arsenal.

No comments:

Post a Comment