Tuesday, August 14, 2012

LIONEL MESSI, CRISTIANO RONALDO, ANDRES INIESTA WACHAGULIWA LEO KUINGIA ‘TOP 3’ YA KUWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA ULAYA


Lionel Messi

Cristiano Ronaldo

Andres Iniesta
MADRID, Hispania
STRAIKA wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo na wachezaji wa Barcelona, Lionel Messi na Andres Iniesta wamechaguliwa leo kuingia ‘top 3’ ya kuwania tuzo ya UEFA ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Ulaya.

Watatu hao walipata pointi nyingi zaidi katika kura zilizopigwa na waandishi wa habari za michezo 53 ambao waliwakilisha vyama vya soka vya kila nchi yenye uanachama wa Shirikisho la Soka la Ulaya (UEFA).

Kiungo mchezeshaji wa Juventus, Andrea Pirlo alikamata nafasi ya nne katika uchaguzi huo, huku kiungo Xavi wa Barcelona, ambaye mwaka jana alikamata nafasi ya pili katika tuzo hiyo, alikamilisha idadi ya 'top 5' kwa kushika nafasi ya tano.

Watatu waliobaki katika mchujo sasa watapigiwa kura Agosti 30  kuamua mshindi wa tuzo hiyo mjini Monaco wakati wa upangaji wa ratiba ya hatua ya makundi ya Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Tuzo huyo binafsi, ilianzishwa kwa ushirikiano wa Chama cha Waandishi wa Habari za Michezo wa Ulaya(ESM), lengo likiwa ni kumtunuku mwanasoka bora, bila kujali utaifa wake, alimradi awe akiichezea klabu iliyo katika nchi yenye uanchama wa UEFA wakati wa msimu uliotangulia.

Messi alikuwa wa kwanza kutwaa tuzo hiyo iliyoanza kutolewa mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment