Friday, August 17, 2012

CASILLAS ASHINDWA KUJIBU NANI KATI YA LIONEL MESSI NA CRISTIANO RONALDO ANAYESTAHILI TUZO MWANASOKA BORA WA DUNIA... AJING'ATANG'ATA WEE, MWISHOOONI ND'O AKAMTAJA RONALDO ETI KWAVILE ANAMJUA SANA...!

Lionel Messi wa Barcelona akimzidi ujanja kipa Iker Casillas wa Real Madrid na kufunga goli huku Cristiano Ronaldo akishuhudia wakati wa mechi ya marudiano ya kuwania taji la Super Cup kwenye Uwanja wa Nou Camp mjini Barcelona, Agosti 17, 2011. Zilifungana 2-2, Barca wakawa vinara kwa ushindi wa jumla wa 4-3.                                                                                                                                                                                                                                                 
Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kufunga goli dhidi ya Barcelona wakati wa mechi yao ya kwanza ya kuwania Kombe la Mfalme kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu jijini Madrid, Januari 18, 2012.  Aliyekalishwa chini kwa goli hilo ni Gerard Pique na anayeshuhudia ni Dani Alves.
Iker Casillas

Cristiano Ronaldo

Lionel Messi
MADRID, Hispania
NAHODHA wa timu ya taifa ya Hispania na klabu ya Real Madrid, Iker Casillas amewaita Lionel Messi na Cristiano Ronaldo kuwa ndio wachezaji bora zaidi duniani kwa sasa na akakiri kwamba sifa za kila mmoja uwanjani zinamfanya ashindwe kujua hadi sasa ni nani kati yao anayestahili kutwaa Tuzo ya Mwanasoka Bora wa Mwaka wa Dunia (FIFA
Ballon d'Or)

Kipa huyo ameendelea kukwepa kutoa msimamo wake juu ya nani atakayemchagua kati ya Messi na Ronaldo, ingawa alikiri kwamba kama uteuzi huo ungefanywa na yeye, basi angemchagua Ronaldo kwa sababu "ndiye anayemjua zaidi."

Akizungumza katika mahojiano na kituo cha televisheni cha Mexico, Univision, Casillas mesema: "Tunawazungumzia wachezaji wawili bora zaidi duniani kwa sasa na swali hili siku zote limekuwa likizua mjadala mkali. Baadhi wanadhani kwamba Messi ndiye bora zaidi, wengine wanaamini kwamba Ronado ndiye anayestahili. Siwezi kumchagua yeyote."

Pamoja na kusema hayo, nyota huyo wa Real Madrid alifichua hatimaye ni nani kati yao anayeweza kumpa nafasi kubwa zaidi ya kutwaa Ballon d'Or.

"Kama nikitakiwa kuchagua mmoja wao, basi atakuwa Cristiano, ni kwa sababu ndiye ninayemjua zaidi kwani tunacheza pamoja katika ngazi ya klabu," amesema.

Casillas aliendelea kusema kwamba yeye anaamini kuwepo kwa wachezaji wawili bora zaidi duniani ni vizuri zaidi kuliko kuwa naye mmoja.

"Tunawazungumzia wachezaji wawili walio bora zaidi duniani kwa sasa, na ninafikiri kwamba kama angekuwa mmoja tu, isingekuwa vizuri sana kwa mchezo wa soka," alihitimisha kipa huyo mwenye miaka 31.

No comments:

Post a Comment