Thursday, August 9, 2012

FERGUSON AKERWA LUCAS MOURA KUWATOSA NA KUFUATA MIJIHELA KIBAO PSG, ASEMA KLABU HIYO YA UFARANSA SASA INAHARIBU SOKA KWA KUMWAGA PESA KIWENDAWAZIMU....!!!

Kwa dau hilo mie basi... ! Kocha Alex Ferguson wa Man U
Lucas Moura... mijihela inayolipwa na PSG imemchanganya Ferguson 
MANCHESTER, England
KOCHA Alex Ferguson ameelezea mshangao wake baada ya Paris Saint-Germain kuishinda Manchester United katika mbio za kutaka kumsajili nyota wa Sao Paulo, Lucas Moura.

Kwa muda mrefu, Man U walikuwa wakipewa nafasi kubwa ya kumnasa yosso huyo mwenye miaka 19, lakini mwishowe mchezaji huyo wa kimataifa wa Brazil akakubali kujiunga na timu hiyo inayosifika kwa kumwaga fedha Ufaransa kwa mkataba wa miaka minne baada ya PSG kukubali kulipa dau nono walilotajiwa la euro milioni 45 (Sh. bilioni 86)

PSG tayari imeshamwaga fedha nyingi kusajili wachezaji kadhaa ghali katika kipindi hiki cha majira ya kiangazi, huku Thiago Silva, Zlatan Ibrahimovic na Ezequiel Lavezzi wote wakikubali kutua kwenye kikosi hicho cha kocha Carlo Ancelotti kinachopigania kutwaa taji lake la kwanza la Ligue 1, Ligi Kuu ya Ufaransa tangu mwaka 1994 na pia kutaka kutwaa ubingwa wa Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya.

Ferguson anaamini kwamba matumizi makubwa ya PSG yanaharibu mchezo wa soka, hata hivyo, akikubali kwamba vigogo hao wa Ufaransa sasa ni wa kuchungwa sana kwani ni miongoni mwa klabu tishio katika soka la Ulaya.

Ameiambia tovuti rasmi ya klabu yake: "Nimeshangazwa kuona kwamba klabu inaweza kulipa hadi euro milioni 45 (Sh. bilioni 86) ili kumsajili mvulana wa miaka 19.

"IIli kumstua kila mmoja, ili kumfahamisha kila mtu kwamba PSG wapo, wamemsajili Thiago Silva na Zlatan Ibrahimovic kutoka AC Milan.

"Lazima watakuwa wameshatumia takriban paundi za England milioni 150 mwezi uliopita. Kma mjuavyo, kikwazo pekee kwa matumizi kama hayo ni UEFA.

"Katika masharti ya soka la Ulaya, hamtafuzu katika michuano ya Ulaya kwa kutwaa ubingwa wa ligi au kumaliza katika nafasi ya pili, mnashiriki pale tu mnapopata mwaliko.

"Hapa ndipo, natumaini iko hivyo, kwamba walau UEFA ina nguvu fulani. Wakati mtu anapolipa euro milioni 45 (Sh. bilioni 86)kwa ajili ya mvulana wa miaka 19, mnapaswa kusema tu kwamba sasa mchezo huu umekuwa wa kiuwendawazimu."

No comments:

Post a Comment