Sunday, August 26, 2012

CRISTIANO RONALDO NOMA...! SASA NDIYE KINARA WA REKODI YA KUWADUNGUA BARCELONA MECHI NNE MFULULIZO WAKIWA KWAO NOU CAMP... AWAPIKU KINA DI STEFANO, RONALDO DE LIMA, ZINEDINE ZIDANE, FIGO...!

Duh... huyu jamaa katupiga tena hapa mara ya 4? Segio Busquet wa Barcelona akijiinamia chini kwa uchungu baada ya Cristiano Ronaldo (anayeshangilia) kumzidi ujanja na kuifungia Real Madrid bao katika mechi yao ya kwanza ya kuwania taji la Super Cup kwenye Uwanja wa Nou Camp, Alhamisi. Hii ilikuwa ni mara ya nne mfululizo kwa Ronaldo kuitungua Barca kwenye uwanja wao wa Naou Camp.   
MADRID, Hispania
Bao la kichwa alilofunga Cristiano Ronaldo Alhamisi dhidi ya Barcelona katika mechi ya kwanza ya 'el clasico' kwenye Uwanja wa Nou Camp kuwania taji la Super Cup limemuongezea rekodi kwa kuwa mchezaji pekee wa Real Madrid kuwahi kuitungua Barca nyumbani kwao katika mechi nne mfululizo.

Rekodi hiyo imumweka Ronaldo kileleni mwa wakali kibao waliowahi kupita Real Madrid wakiwamo magwiji kama Di Stefano, Zinedine Zidane 'Zizzou', Ronaldo De Lima na hata Mreno mwenzake Luis Figo. 

Ronaldo aliidungua Barca Agosti mwaka jana katika mechi ya Super Cup, akawatandika tena Januari, 2012 katika mechi ya marudiano ya Kombe la Mfalme, April, 2012 akapiga goli 'kali' la ushindi wakati Real iliposhinda 2-1 katika marudiano ya mechi ya La Liga, Ligi Kuu ya Hispania msimu uliopita na Alhamisi iliyopita, akafunga tena wakati wakilala 3-2 katika mechi ya kwanza ya taji la Super Cup la Hispania.



Real Madrid watarudiana na Barcelona kuwania taji la Super Cup Jumatano kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu. 

No comments:

Post a Comment