Thursday, August 9, 2012

ONA CAZORLA, GIROUD, PODOLSKI WAKIJIFUA NA ARSENAL UJERUMANI

"Jembe" jipya la Gunners, Santiago Cazorla likishiriki mazoezi na timu yake ya Arsenal nchini Ujerumani ambako wameenda kwa ajili ya kambi ya maandalizi ya msimu mpya.

Ngoja nipashe ya mwisho mwisho kabla sijaenda Man United... Robin van Persie naye pia ameambatana na timu Ujerumani licha ya Sir Alex Ferguson kuthibitisha leo kwamba Manchester United imetuma ofa ya paundi milioni 15 kwa ajili ya kumsajili. Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger amesema Mholanzi huyo anauzwa paundi milioni 20.

Huyu naye anatakiwa na Barcelona... Alex Song akipozi kwa picha wakati wa mazoezi ya Arsenal nchini Ujerumani
Sijui nibaki hapa.....!?  RVP akishiriki mazoezi nchini Ujerumani

Msimu mpya si uanze tu, nina usongo.... Kiungo mpya wa Arsenal, Santiago Cazorla akiwa mazoezini na Arsenal nchini Ujerumani

Ngoja nipozi kwa picha... huyu ni Theodore Walcott
Mashine nyingine mpya... Lukas Podolski (kulia) akisimama jirani na Oxlade-Chamberlain
Pasha baba.... Cazorla akipasha
Ngoja nijipumzikie mie sina haja ya kujitesa kujua mbinu zake yule babu Wenger, maana sitarajii kuzitumia nikiwa Man United... RVP akipumzika
Yule RVP yaani nimemvumiliaaa wakati akisumbuliwa na majeraha kila mwaka, leo kapona ananiletea pozi, ntamnyima "razi" akafulie kama Hleb... Kocha Arsene Wenger akishiriki mazoezi ya Arsenal nchini Ujerumani.
Van Persie wewe ondoka tu mi nipate namba ya uhakika, nisije nikawa kama Chamakh bureee... Mshambuliaji mpya wa Arsenal, Olivier Giroud akishiriki mazoezi ya timu hiyo nchini Ujerumani
Ha ha haaaa.... Anatuchekesha sana RVP na hizo "nataka-sitaki" zake... Mabeki wa Arsenal, Laurent Koscielny (kushoto) na Verminator wakifurahia jambo wakati wa mazoezi ya timu yao nchini Ujerumani 
Kama Usain Bolt kudadadeki... Verminator akitoka nduki wakati wa mazoezi ya Arsenal nchini Ujerumani
Lazima uwe ngangari hapa, hata wakisvuta shati wewe uwe unakimbia tu... Cazorla (kulia) akikimbia huku akivutwa nyuma wakati wa mazoezi ya Arsenal nchini Ujerumani
Sijatwaa makombe miaka kibao, mwaka huu nikikosa tena naona watanitimua... Babu Wenger akiondoka uwanjani baada ya kumalizika kwa mazoezi
Santi Cazorla akipasha
Wachezaji wa Arsenal nchini Ujerumani
Mwenzenu hapa niko kwetu.... Lukas Podolski akifurahi wakati wa mazoezi ya Arsenal nchini kwao Ujerumani
RVP
Santiago Cazorla
Kiberenge cha Arsenal hiki... Alex Oxlade Chamberlain

No comments:

Post a Comment