Monday, August 20, 2012

BILA NYIE ISINGEWEZEKANA... VILLA AREJEA ATUPIA, MESSI APIGA 2, BARCA YAUA 5-1, REAL YASHIKWA 1-1, RONALDO HOI...

Mshambuliaji wa Barcelona, David Villa akishangilia goli lake alilofunga dhidi ya Real Sociedad kwa kuonyesha fulana yake yenye picha ya familia yake, inayosomeka: "Bila ya nyie isingewezekana", ambapo alikimbilia kuwakumbatia madaktari wa timu hiyo kwenye Uwanja wa Nou Camp mjini Barcelona jana usiku Agosti 19, 2012. Villa, ambaye alikaa nje ya uwanja kwa tangu alipovunjika mguu Desemba mwaka jana, aliruhusiwa kucheza na madaktari wa Barca mwezi uliopita. Picha: REUTERS

Mshambuliaji wa Barcelona, David Villa akishangilia goli lake alilofunga dhidi ya Real Sociedad kwa kuonyesha fulana yake yenye picha ya familia yake, inayosomeka: "Bila ya nyie isingewezekana", ambapo alikimbilia kuwakumbatia madaktari wa timu hiyo kwenye Uwanja wa Nou Camp mjini Barcelona jana usiku Agosti 19, 2012. Villa, ambaye alikaa nje ya uwanja kwa tangu alipovunjika mguu Desemba mwaka jana, aliruhusiwa kucheza na madaktari wa Barca mwezi uliopita. Picha: REUTERS
Lionel Messi akiwafungisha tela wachezaji wawili wa Real Sociedad wakati wa mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Hispania kwenye Uwanja wa Nou Camp mjini Barcelona jana usiku Agosti 19, 2012. Messi alitupia mbili, Puyol moja, Pedro moja na David Villa moja.
Dah mambo haya yakiendelea tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia ntaipata kweli... Straika wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo akijiuliza baada ya kupoteza nafasi ya kufunga wakati wa mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Agosti 19, 2012. Real walitoka 1-1, huku goli la Real likifungwa na Higuain. Picha: REUTERS

Mastraika wa Real Madrid, Gonzalo Higuain (kushoto) na Karim Benzema wakitoka uwanjani baada ya mechi yao ufunguzi wa Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Agosti 19, 2012. Real walianza kutetea ubingwa wao wa La Liga kwa fadhaa baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya Valencia, licha ya kutawala mechi nzima kwenye Uwanja wa Bernabeu. Picha: REUTERS
Kipa wa Real Madrid, Iker Casillas akisikitika wakati wa mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Hispania (La Liga) dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana Agosti 19, 2012. Real walitoka 1-1, huku goli la Real likifungwa na Higuain. Picha: REUTERS

Kocha wa Valencia, Mauricio Pellegrino (kushoto) akimsalimia kocha wa Real Madrid, Jose Mourinho kabla ya mechi yao ya ufunguzi wa Ligi Kuu ya Hispania dhidi ya Valencia kwenye Uwanja wa Santiago Bernabeu mjini Madrid jana usiku Agosti 19, 2012. Real walianza kutetea ubingwa wao wa La Liga kwa fadhaa baada ya kulazimishwa sare ya 1-1 nyumbani dhidi ya Valencia, licha ya kutawala mechi nzima kwenye Uwanja wa Bernabeu. Picha: REUTERS

No comments:

Post a Comment