Friday, July 6, 2012

Azam yapiga la tatu. Ni 3-2. LIVE KUTOKA Z'BAR

SOMOE NG'ITU ANARIPOTI LIVE KUTOKA ZANZIBAR

Dk. 82. Ni 3-2. Azam yazinduka. Ibrahim Mwaipopo ameifungia Azam bao 3 dhidi ya Mafunzo.

Mafunzo waliotanguliwa kwa 2-0 walisawazisha yote mawili kupitia kwa Sadick na Mohammed Abdulrahman na kufanya ngoma kuwa 2-2 katika mechi yao ya tatu ya Kombe la Urafiki.

Ramadhani Chombo "Redondo"  alitupia la kwanza mapema kipindi cha kwanza na Kipre Tchetche akaongeza la pili katika dakika ya 34.

Katika mechi ya kwanza, Azam walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Karume Boys (U23) ya Zanzibar kabkla ya kutoka sare ya 1-1 tena dhidi ya Simba.

Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba leo watacheza mechi ya pili usiku dhidi ya Karume Boys (U23) ya Zanzibar.

Katika mechi ya kwanza Simba waliibwaga Mafunzo kwa mabao 2-0 kabla ya kutoka sare ya 1-1 na Azam.

No comments:

Post a Comment