Wednesday, July 11, 2012

RAIS KIKWETE ATUA LONDON NA KUZUNGUMZA NA WACHEZAJI WA TIMU YA TAIFA ITAKAYOSHIRIKI OLIMPIKI

Hapa Rais Kikwete (katikati) akiwa katika picha ya pamoja na wachezaji wa timu hiyo ya taifa itakayoshiriki Olimpiki, leo jijini London.   

JK, mama Salma JK na Balozi wa Tanzania, England, Peter Kallaghe (wa sita kutoka kushoto) wakiwa katika picha ya pamoja na wachezaji na maafisa wa timu ya taifa itakayoshiriki Olimpiki, leo jijini London. 

Rais JK akizungumza leo jijini London na wachezaji na maafisa wa timu ya taifa itakayoshiriki Olimpiki.

JK akiteta leo jijini London na Balozi Kallaghe wakati akizungumza na wachezaji wa timu ya taifa itakayoshiriki Olimpiki.
LONDON, England
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Jakaya Kikwete, leo amekutana na wachezaji sita wanaounda kikosi cha timu ya taifa ya michezo mbalimbali iliyopo jijini London kushiriki michezo ya Olimpiki kuanzia Julai 26.

Katika mazungumzo hayo, Rais JK aliyekuwa na mkewe, Mam Salma Kikwete, aliwapa moyo wachezaji hao na kuwataka wajitahidi kupeperusha vyema bendera ya taifa na ikibidi warejee nchini na medali. Rais JK yupo England kwa ziara ya kikazi.

No comments:

Post a Comment