Tuesday, July 31, 2012

MAHAKAMA KUU YASHINDWA LEO KUTOA UAMUZI KUHUSU MGOMO WA WALIMU


Rais wa CWT, Gratian Mukoba (kushoto)
Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Ufundi, Dk. Shukuru Kawambwa
Mahakama Kuu Divisheni ya Kazi katika Kanda Maalum ya Dar es Salaam imeshindwa kutoa uamuzi wa mgogoro uliopo baina ya serikali na walimu na ambao ndio uliozaa mgomo wa walimu usio na kikomo kwa nchi nzima kuanzia jana.  

Jaji Sophy Wambura wa Mahakama hiyo aliahirisha shauri hilo hadi Alhamisi (Agosti 2) wakati atakapolitolea uamuzi baada ya kupitia hoja za pande zote mbili .    

Awali, wakili wa serikali aliiomba mahakama hiyo kukiamuru Chama Cha Walimu Tanzania (CWT) kusitisha mgomo huo ulioanza jana kwani ni batili.

Wakili wa CWT alisema kuwa mgomo huo ni halali kwani umefuata sheria na taratibu zote kabla ya kuitishwa kwake.

CWT iliitisha mgomo wa walimu kuanzia jana baada ya mgogoro wake na serikali kushindwa kupatiwa ufumbuzi na msuluhishi.

Chama hicho kinataka serikali iongeze mshahara wa walimu kwa asilimia 100, kuongeza posho za walimu kwa asilimia 50 na 55 kwa walimu wa sayansi na pia kuwalipa walimu posho ya mazingira magumu kwa kiasi cha asilimia 30 ya mshahara.

No comments:

Post a Comment