Thursday, July 26, 2012

CAPELLO AWA KOCHA WA URUSI, AAHIDI MAKUBWA


Fabio Capello
MOSCOW, Urusi
KOCHA wa zamani wa timu ya taifa ya England, Fabio Capello ameapa kubadili soka la Urusi na kuifanya timu ya taifa hilo kuwa moja ya timu kali duniani ikiwa ni muda mfupi tu baada ya kusaini mkataba wa miaka miwili wa kuifundisha timu hiyo leo.

Muitalia Capello anachukua nafasi ya Mholanzi Dick Advocaat, ambaye kibarua chake kiliota mbawa kufuatia matokeo mabaya waliyopata Urusi katika fainali za Euro 2012, ambazo waliishia katika hatua ya makundi.

Kocha huyo mwenye miaka 66, alionekana akiwa amevalia suti ya kijivu na tai ya bluu nyeusi. Hakuchelewa kuahidi mbele ya waandishi wa habari jijini Moscow kwamba atafanya kazi yake kwa ukamilifu.

"Najivunia kuwa kocha wa timu ya taifa ya Urusi. Kuna vipaji vingi Urusi. Nitaishi na kufanya kazi jijini Moscow," alisema.

Taarifa za vyombo vya habari vya Urusi zimedai kuwa atakuwa akilipwa mshahara wa euro milioni 10 kwa mwaka (Sh. bilioni 20)

No comments:

Post a Comment