HISPANIA,
ITALIA ZAPETA EURO 2012
Mario Balotelli wa Italia (wa
pili kulia) akishangilia na wachezaji wenzake baada ya kufunga goli dhidi ya Ireland
usiku huu.
|
WARSAW,
Poland
MABINGWA
watetezi Hispania wamemaliza kileleni mwa Kundi C usiku huu baada ya kushinda
1-0 dhidi ya Croatia wakati Italia waliungana nao pia kufuzu kwa hatua ya robo
fainali ya Euro 2012 kutokana na ushindi wao wa mabao 2-0 dhidi ya Ireland.
Hispania
walikuwa na hatihati ya kuadhiriwa katika mechi yao mjini Gdansk ambako bao la
kutangulia la Croatia lingeweza kuwang'oa katika fainali hizo, lakini Jesus
Navas aliwafungia goli la 'usiku' wakati zikiwa zimebaki dakika mbili kabla
mechi kumalizika na kuwaweka kileleni mwa msimamo ambapo sasa watacheza dhidi
ya timu itakayoshika nafasi ya pili kwenye msimamo wa Kundi D.
Katika
mechi ya jana, Hispania walimiliki mpira kwa asilimia 76 na kupiga mashuti 14
dhidi ya mashuti matano ya Croatia.
Waitalia
walifunga bao lao la kwanza katika dakika ya 35 mjini Poznan wakati mpira wa
kichwa wa Antonio Cassano aliounganisha kutokana na kona ulivuka mstari wa goli
na shaka yao ya kushikiliwa na Ireland waliokuwa tayari wameshatolewa
ilimalizwa na goli 'kali' la Mario Balotelli muda mfupi baada ya Keith Andrews
wa Ireland kutolewa nje kwa kadi nyekundu.
Kwa
ushindi huo, Italia sasa watacheza mechi yao ya robo fainali dhidi ya timu
itakayomaliza kileleni mwa Kundi D, ambalo hadi sasa linaongozwa na Ufaransa na
mechi zake zitahitimishwa leo Jumanne.
Katika
mechi za Kundi D leo, Sweden watacheza dhidi ya Ufaransa na wenyeji Ukraine
watawavaa England, zote zikichezwa kuanzia saa 3:45 usiku.
No comments:
Post a Comment