Monday, June 18, 2012


LEBRON AIPAISHA MIAMI NBA

LeBron James


MIAMI, Marekani
TIMU ya mpira wa kikapu ya Miami Heat imeifunga Oklahoma City Thunder kwa pointi 91-85 na kutwaa uongozi wa 2-1 katika mechi ya tatu ya mfululizo wa mechi saba za fainali ya Ligi ya Mpira wa Kikapu Marekani (NBA) juzi.
LeBron James aliongoza katika ufungaji baada ya kufunga pointi 29, Dwyane Wade akaongeza nyingine 25 kwa Miami huku nyota wa Oklahoma, Kevin Durant akifunga pia pointi 25. Mechi yao ya nne itachezwa kesho mjini Miami.

No comments:

Post a Comment