Saturday, June 30, 2012

GUARDIOLA ATAMANI KIBARUA


Guardiola akionyesha tuzo aliyotwaa ya Kocha Bora wa Mwaka wa Dunia 2011 

KUALA LUMPUR, Malaysia
Pep Guardiola amekiri kwamba tayari ameanza kuhisi kuwa ‘amemisi’ soka ikiwa ni wiki chache tu baada ya kujiondoa katika nafasi ya kuwa kocha wa Barcelona.

Kocha huyo aliyeandika rekodi ya kuwa  mwenye mafanikio kuliko wote waliowahi kuifundisha Barca,  aliamua kutosaini mkataba mwingine wa kumbakisha Camp Nou baada ya kudumu kwa miaka minne, akidai kwamba uchovu ndio sababu kubwa ya kuondoka kwake.
Hata ahivyo, kocha huyo mwenye miaka 41 amesema kwamba tayari ameanza kutamani kurejea katika masuala ya soka, kabla hajatania kwa kusema kuwa ameshachoka kuendelea kucheza gofu.

"Ninatamani soka? Kiukweli nimeanza kulimisi soka. Nimeshachoka kucheza gofu na baba yangu," Pep aliwaambia waandishi wa habari wakati wa ziara yake mjini Kuala Lumpur, Malaysia.

Guardiola aliiongoza Barca kutwaa mataji 14 wakati wa kipindi chake cha miaka minne. Nafasi yake imerithiwa na aliyekuwa msaidizi wake, Tito Vilanova na kwa muda mrefu amekuwa akihusishwa na uhamisho wa kwenda Chelsea.

No comments:

Post a Comment