Friday, February 22, 2013

PELE: NEYMAR ANACHOJALI NI KUBADILI MITINDO YA NYWELE TU

Neymar
Neymar
Neymar

Neymar
Neymar

Neymar

Neymar wa Santos akifungishwa tela na Lionel Messi wa Barcelona wakati wa mechi yao ya fainali ya Kombe la Dunia la Klabu kwenye Uwanja wa Yokohama International mjini Yokohama, Japan Desemba 18, 2011.
Neymar wa timu ya taifa ya Brazil na Gary Cahill (kulia) wa timu ya taifa ya England wakiwania mpira wakati wa mechi yao ya kirafiki ya kimataifa kwenye Uwanja wa Wembley mjini London, England Februari 6, 2013.
Neymar wa timu ya taifa ya Brazil na Glen Johnson wa timu ya taifa ya England wakiwania mpira wakati wa mechi yao ya kirafiki ya kimataifa kwenye Uwanja wa Wembley mjini London, England Februari 6, 2013.

Neymar wa timu ya taifa ya Brazil akikontroo mpira huku akichungwa na Tom Cleverley wa timu ya taifa ya England wakati wa mechi yao ya kirafiki ya kimataifa kwenye Uwanja wa Wembley mjini London, England Februari 6, 2013.

MSHINDI mara tatu wa Kombe la Dunia, Pele, ameanzisha mashambulizi dhidi ya Mbrazil mwenzake, Neymar, akisema anacheza chini ya kiwango anapoiwakilisha timu yake ya taifa na kwamba anachojali zaidi ni mwonekano wake tu.

Mshambuliaji huyo mwenye umri wa miaka 21 amekuwa akilinganishwa na Pele, lakini gwiji huyo mwenye umri wa miaka 72, ambaye daima alikuwa akidai kwamba Neymar ni bora kuliko mwanasoka bora wa dunia mara nne mfululizo, Lionel Messi, amemgeuka akidai yosso huyo anapewa sifa kubwa mno kuliko anazostahili.

"Kwa timu ya taifa, yeye ni mchezaji wa kawaida sana," Pele aliliambia gazeti la O Estado de Sao Paulo.

"Ana majukumu makubwa lakini anachojali ni kubadili ni staili yake na mitindo ya nywele.

"Kila mechi tunayoenda kucheza nje ya nchi, hachezi vizuri. Kila mtu anadhani kwamba yeye ndiye anayepaswa kuwa jibu la matatizo yetu yote yaliyopo kwenye timu yetu ya taifa [lakini] Neymar hayuko tayari kubebeshwa mzigo mkubwa kiasi hicho, hawezi kuubeba."

Pele kisha akaongeza kwamba anaamini kuwa kiwango cha kufadhaisha cha Neymar kwenye timu ya taifa ya Brazil, ambacho ni tofauti na anachoonyesha kila siku akiwa na klabu yake ya Santos, ambako ameshatwaa Kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Amerika Kusini la "Copa Libertadores", linatokana na kukosa uzoefu wa mbinu za Ulaya.

"Hajawahi kucheza soka nje ya nchi, na soka la Ulaya ni tofauti na tunalocheza hapa Amerika Kusini," aliendelea.

"Anapenda kukaa na mpira, kupiga chenga, kuonyesha mbwembwe zake [lakini] anapaswa kuuacha mpira kidogo, acheze kwa ajili ya timu.

"Hana uzoefu kabisa wa kimataifa. Barcelona itakuwa ni timu nzuri kwake [lakini] sijui kama ataondoka kwa sababu Santos bado wanamuhitaji."

No comments:

Post a Comment