Friday, July 6, 2012

AZAM YAONGOZA 2-0: LIVE KUTOKA ZANZIBAR

Ramadhani Chombo 'Redondo' mfungaji wa bao la kwanza la Azam katika mechi ianyoendelea kwenye Uwanja wa Amaan, Zanzibar

SOMOE NG'ITU ANARIPOTI LIVE KUTOKA ZANZIBAR

ZANZIBAR kipindi cha pili kinaanza. Azam wanaongoza 2-0 dhidi ya Mafunzo katika mechi yao ya Kombe la Urafiki.

Ramadhani Chombo "Redondo"  alitupia la kwanza mapema kipindi cha kwanza na Kipre Tchetche akaongeza la pili katika dakika ya 34.


Katika mechi ya kwanza, Azam walitoka sare ya 1-1 dhidi ya Karume Boys (U23) ya Zanzibar kabkla ya kutoka sare ya 1-1 tena dhidi ya Simba.
 
Mabingwa wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara, Simba leo watacheza mechi ya pili usiku dhidi ya Karume Boys (U23) ya Zanzibar.

Katika mechi ya kwanza Simba waliibwaga Mafunzo kwa mabao 2-0 kabla ya kutoka sare ya 1-1 na Azam. 

No comments:

Post a Comment