Thursday, June 21, 2012


SEERDOF AONDOKA AC MILAN

Clarence Seedorf


Milan, Italia
AC Milan wamekubali kuwasajili beki wa Chievo, Francesco Acerbi na kiungo wa Genoa, Kevin Constant lakini kiungo wao Clarence Seedorf anaondoka katika klabu hiyo ya Serie A, Ligi Kuu ya Italia baada ya kuitumikia kwa miaka 10, imefahamika.

Milan, waliovuliwa ubingwa wao wa Italia na Juventus mwezi Mei, wanajenga upya kikosi chao baada ya kuondoka kwa nyota kadhaa ‘wazee’ wakiwemo Gennaro Gattuso, Alessandro Nesta, Filippo Inzaghi, Gianluca Zambrotta na Mark van Bommel.

Mholanzi Seedorf, aliyeng’ara katika fainali za Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya mwaka 2003 na 2007 wakati Milan ikitwaa medali nne za ushindi, ameungana na kundi la wanaoondoka lakini hakusema ni wapi anakwenda licha ya uvumi kuenea kuwa atajiunga na klabu ya Botafogo ya Brazil.

"Kwakweli namshukuru kila mmoja," kiungo huyo mwenye miaka 36 na ambaye hakucheza mechi nyingi msimu uliopita, aliuambia mkutano na waandishi wa habari leo.

"Nitawaeleza hatma yangu hivi karibuni. Naondoka. Ninatakiwa na timu nyingi sana," aliongeza mchezaji huyo amabaye anakabidhi jezi yake namba 10 ya Milan kwa mshambuliaji wa kimataifa wa Sweden, Zlatan Ibrahimovic.


No comments:

Post a Comment