Sunday, October 7, 2012

MBWANA SAMATTA, TRESSOR MPUTU WATOSWA KATIKA ORODHA YA NYOTA 34 WANAOWANIA TUZO YA MWANASOKA BORA WA AFRIKA 2012... WAMEJAA 'MAPROO' WA ULAYA KAMA YAYA TOURE, DEMBA BA, GERVINHO, PAPISS DEMBA CISSE ... WANAOCHEZA AFRIKA NI WATATU TU AMBAO NI MSAKNI WA ESPERANCE YA TUNISIA, RAINFORD KIDIABA NA STOPHILA SUNZU WA TP MAZEMBE YA DR CONGO


Mbwana Samatta
Tressor Mputu
Yaya Toure
CAIRO, Misri
Shirikisho la Soka la Afrika (CAF) limetaja majina ya awali ya wachezaji nyota 34 barani wanaowania tuzo ya Mwanasoka Bora wa Afrika Mwaka 2012 ambamo ndani yake, wamejaa 'maproo' 29 wanaocheza soka la kulipwa nje ya Afrika huku nyota wa TP Mazembe, Mtanzania Mbwana Samatta na Tressor Mputu wanaong'ara katika Ligi ya Klabu Bingwa Afrika wakikosekana kwenye orodha hiyo.

Miongoni mwa wanaocheza soka la kulipwa Ulaya ni mshindi wa tuzo hiyo msimu uliopita, kiungo wa timu ya taifa ya Ivory Coast na klabu ya Manchester City ya England, Yaya Toure, mastraika nyota wa Newcastle United -- Papiss Demba Cisse na Demba Ba na pia winga wa Arsenal, Gervinho..

Wachezaji watatu wanaocheza katika klabu za Afrika ni Wazambia Rainford Kalaba na Stoppila Sunzu wanaoichezea TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Youssef Msakni wa Esperance ya Tunisia.

Orodha kamili:
1.    Abdelaziz Barrada - Getafe (Hispania) na Morocco

2.    Adel Taarabt - Queens Park Rangers (England) na Morocco

3.    Alain Sibiri Traore - Lorient (Ufaransa) na Burkina Faso

4.    Alexander Song - Barcelona (Hispania) na Cameroon

5.    Andre 'Dede' Ayew - Marseille (Ufaransa) na Ghana

6.    Arouna Kone - Wigan (England) na Ivory Coast

7.    Aymen Abdennour - Toulouse (Ufaransa) na Tunisia

8.    Bakaye Traore - AC Milan (Italia) na Mali

9.    Cheick Tiote - Newcastle United (England) na Ivory Coast

10.    Christopher Katongo - Henan Construction (China) na Zambia

11.    Demba Ba - Newcastle United (England) na Senegal

12.    Didier Drogba - Shanghai Shenhua (China) na Ivory Coast

13.    Emmanuel Agyemang-Badu - Udinese (Italia) na Ghana

14.    Emmanuel Mayuka - Southampton (England) na Zambia

15.    Foxi Kethevoama - FC Astana (Kazakhstan) na Afrika ya Kati.

16.    Gervinho - Arsenal (England) na Ivory Coast

17.    Hilaire Momi - Le Mans (Ufaransa) na Afrika ya Kati.

18.    John Obi Mikel - Chelsea (England) na Nigeria

19.    John Utaka - Montpellier (Ufaransa) na Nigeria

20.    Kwadwo Asamoah - Juventus (Italia) na Ghana

21.    Moussa Sow - Fenerbahce (Uturuki) na Senegal

22.    Nicolas N'koulou - Marseille (Ufaransa) na Cameroon

23.    Papiss Demba Cisse - Newcastle United (England) na Senegal

24.    Pape Moussa Konate - FC Krasnodar (Urusi) na Senegal

25.    Pierre-Emerick Aubameyang - St Etienne (Ufaransa) na Gabon

26.    Rainford Kalaba - TP Mazembe (DR Congo) na Zambia

27.    Seydou Doumbia - CSKA Moscow (Urusi) na Ivory Coast

28.    Seydou Keita - Dalian Aerbin (China) na Mali

29.    Sofiane Feghouli - Valencia (Hispania) na Algeria

30.    Stoppila Sunzu - TP Mazembe (DR Congo) na Zambia

31.    Victor Moses - Chelsea (England) na Nigeria

32.    Yaya Toure - Manchester City (England) na Ivory Coast

33.    Younes Belhanda - Montpellier (Ufaransa) na Morocco

34.    Youssef Msakni - Esperance (Tunisia) na Tunisia

No comments:

Post a Comment