TETESI ZA USAJILI
Robin van Persie |
VAN PERSIE ATAKIWA MAN U, BARCA
MANCHESTER City watatuma maombi ya kutaka kumsajili straika wa Arsenal,
Robin Van Persie, 28, kwa ada ya uhamisho ya paundi milioni 15, lakini Barcelona na Paris Saint-Germain pia wanamuwania mchezaji huyo, ambaye ameamua hatasaini mkataba mpya.
Habari kamili: the Sun
AC MILAN PIA WAMHITAJI RVP
VITA ya kumuwania Van Persie imeongezeka baada ya AC Milan kuingia katika mbio za kutaka kumsajili Mholanzi huyo.
Habari kamili: The Times (kwa kulipia)
MANCHESTER City watatwaa kombe la Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kama Robin van Persie atatua Etihad Stadium, kwa mujibu wa beki wa City, Kolo Toure.
Habari kamili: Daily Telegraph
BEKI wa zamani wa Arsenal, Sol Campbell, 37, ameiambia klabu yake ya zamani kwamba njia pekee ya kumbakisha Van Persie ni kutumia paundi milioni 100 katika kununua wachezaji wapya wa kiwango cha dunia.
Habari kamili: Daily Mirror
MWENYEKITI wa Arsenal, Peter Hill-Wood amesema shutuma dhidi ya klabu hiyo inavyoendeshwa ni "upuuzi mtupu".
Habari kamili: the Guardian
NAHODHA wa Manchester United, Nemanja Vidic, 30, anatumai kwamba atakuwa fiti kwa ajili ya mwanzo wa msimu baada ya kurejea mazoezini na kikosi cha kwanza.
Habari kamili: Daily Mail
ANELKA ATAKA KUREJEA ENGLAND
NICOLAS Anelka, 33, anapanga kurejea kwenye ligi kuu ya England baada ya mahusiano yake na Shanghai
Shenhua kuwa mabaya, kutokana na kutofautiana na mashabiki.
Full story: Metro
LIVERPOOL YAKARIBIA KUMNASA STRAIKA WA ROMA
KOCHA Brendan Rodgers anakaribia kumsajili straika wa Roma, Fabio Borini, 21, ili awe mchezaji wa kwanza kumsajili tangu akabidhiwe mikoba ya kuifundisha klabu hiyo ya Anfield.
Habari kamili: Daily Telegraph
HAbari kamili: Daily Mail
MODRIC AKARIBIA KUTUA REAL MADRID
LUKA Modric, 26, anakaribia kuafiki dili la uhamisho litakalogharimu paundi milioni 28 ili kuhama kutoka White Hart Lane na kutua Real Madrid.
Habari kamili: talkSPORT
NEWCASTLE YAMKATAA "FUNDI" HOILETT
NEWCASTLE imekataa fursa ya kumsajili winga 'fundi' wa kuwapunguza mabeki Junior Hoilett, 22, kutoka Blackburn, lakini wanakaribia kumsajili mchezaji yosso wa timu ya taifa ya vijana ya Australia ya U-20, Curtis Good, 19, kutoka Melbourne Heat.
Habari kamili: Newcastle Chronicle
No comments:
Post a Comment