Tuesday, July 3, 2012

TAKUKURU YAJITOSA KUCHUNGUZA VIGOGO WALIOFICHA ‘MIHELA’ USWISI


Mkurugenzi wa TAKUKURU, Dk. Edward Hosea
Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa nchini (TAKUKURU) imeanza uchunguzi mkali dhidi ya vigogo wanaodaiwa kuficha Uswisi mabilioni ya fedha walizopata kwa njia haramu.

Waziri wa Nchi katika Ofisi ya Rais (Utawala Bora), George Mkuchika, ametoa taarifa hizo Bungeni mjini Dodoma leo wakati akijibu hoja mbalimbali za wabunge kabla ya kuhitimisha mjadala kuhusu makadirio na matumizi ya wizara yake kwa mwaka ujao wa fedha.
Mkuchika alisema kuwa hadi sasa, tayari TAKUKURU imeanza kushughulikia tuhuma hizo kwa kuwasiliana na watu wa Uswisi ili mwishowe undani wa jambo hilo ufahamike na hatua stahili kuchukuliwa.

Awali, wabunge mbalimbali waliitaka Serikali kufanya uchunguzi juu ya madai kwamba wapo vigogo mbalimbali serikalini walijilimbikizia zaidi ya Sh. bilioni 300 nchini Uswisi na kwamba, ‘mihela’ hiyo imepatikana kwa njia zisizo halali, zikiwemo zilizopatikana kupitia baadhi ya mikataba ya utafutaji mafuta na gesi ambayo mwishowe italigharimu taifa.


No comments:

Post a Comment