Monday, July 2, 2012

REKODI KALI ZILIZOWEKWA WAKATI HISPANIA WAKITWAA UBINGWA EURO 2012


Casillas kweli mnoko… ! Hebu muangalie (katikati) anavyombania Mario Balotelli kuifungia Italia walau bao moja la kichwa ili wajipoze kutokana na kichapo kikali walichowapa jana. Kulia, anayeshuhudia ukuda wa Casillas ni Sergio Ramos.

Kutoka kushoto ni Gerard Pique, Pepe Reina, Fernando Llorente, Iker Casillas na Xavi Hernandez wakishangilia kombe walilotwaa baada ya kuinyoa Italia 4-0 jana.

Dah... inaelekea chama hili litanifanya nibebe makombe hadi makwapa kuniuma!
Nahodha wa Hispania, Iker Casillas (kulia) akishikilia vizuri kombe la UEFA Euro 2012 huku akitazamwa na kocha wao, Vicente del Bosque (kulia). Hapa ni wakati wakitoka ndani ya pipa baada ya kutua kwenye Uwanja wa Ndege wa Barajas jijini Madrid, leo.
KIEV, Ukraine
IFUATAYO ni orodha ya rekodi mbalimbali za kukumbukwa baada ya Hispania kuifunga Italia mabao 4-0 katika mechi yao ya fainali ya Euro 2012.

* Hispania wamekuwa timu ya kwanza kutwaa mara mbili mfululizo taji la Ulaya huku pia wakiwa mabingwa wa Kombe la Dunia. Taji hilo la Euro lilikuwa la tatu kwa Hispania, hivyo kufikia rekodi ya Ujerumani ambayo pia imewahi kubeba kombe hilo mara tatu.

* Ushindi wa tofauti ya mabao manne ulikuwa ndio mkubwa kuliko yote katika historia ya fainali za Ulaya na pia Kombe la Dunia.

* Vicente Del Bosque ni kocha wa pili tu aliyewahi kutwaa kwa mpigo mataji ya Euro na Kombe la Dunia, akiungana na Helmut Schoen, aliyeiongoza Ujerumani Magharibi kutwaa ubingwa wa Ulaya mwaka 1972 na kubeba Kombe la Dunia miaka miwili baadaye.

* Ushindi wa juzi wa Hispania ulikuwa ndio wa kwanza dhidi ya Italia katika kwa miaka nane katika mechi za michuano mikubwa (walishinda kwa penati baada ya sare ya 0-0 katika robo fainali ya Euro 2008)

* Straika Fernando Torres amekuwa mchezaji wa kwanza kufunga katika fainali mbili za michuano ya Euro na kutwaa kiatu cha dhahabu kwa kuwa mfungaji bora wa Euro 2012, akibebwa na pasi yake ya bao na pia kucheza kwa dakika chache zaidi ya Mario Gomez ambaye pia aliufikisha mabao matatu.

* Hispania hawajawahi kufungwa katika mechi 12 zilizopita za fainali ya Euro na pia hawakuruhusu goli katika mechi zao tano zilizopita, takwimu zote hizo zikiwa ni rekodi ya michuano hiyo. Hawajawahi kufungwa katika mechi zao 10 za mtoano kwenye fainali za Euro na Kombe la Dunia.

* Kipigo chao cha mwisho katika mechi ya fainali za Euro kilikuwa ni cha 2-0 kutoka kwa Sweden wakati wa kuwania kufuzu fainali za mwaka 2006, wakati huo ikiwa ni baada ya kucheza mechi 29 mfululizo bila kufungwa.

* Mara ya mwisho Hispania kufungwa baada ya kuongoza kwa bao 1-0 walilala kwa mabao 3-2 kutoka kwa Ireland ya Kaskazini, Septemba mwaka 2006.

* Juzi ilikuwa ni mara ya tatu kwa timu kuongoza kwa 2-0 kabla ya mapumziko katika mechi ya fainali ya Euro. Italia iliifunga Yugoslavia 2-0 mwaka 1968 na Czechoslovakia waliichapa Ujerumani Magharibi kwa penati mwaka 1976 baada ya kuongoza 2-1 hadi kufikia mapumziko.

* Kipa wa Hispania, Iker Casillas amekuwa mchezaji wa pili tu, pamoja na gwiji wa Ujerumani Franz Beckenbauer (1972-1976) kuwa nahodha wa timu ya taifa aliyeiongoza nchi yake katika fainali tatu za Euro/Kombe la Dunia.

* Casillas pia ni mchezaji wa kwanza kushinda mechi 100 za kimataifa na pia ana rekodi ya kutofungwa katika mechi 79 kati ya 136 alizoichezea timu yake ya taifa.

* Kiungo wa Hispania, David Silva alihusika moja kwa moja katika mabao matano ya Euro 2012 (akifunga magoli 2, akitoa pasi 3 za mabao), idadi ambayo ni kubwa kuliko wachezaji wote.

* Kipa Gianluigi Buffon wa Italia alivunja rekodi ya Dino Zoff ya kucheza mechi nyingi za fainali za Euro/Kombe la Dunia baada ya kucheza mechi ya 25 juzi. Ni Paolo Maldini (mechi 36) na Fabio Cannavaro (mechi 26) ndio wanaompita kwa idadi ya mechi alizoichezea Italia.

No comments:

Post a Comment