Kama nyani vile...! Casillas akifanya vitu vyake wakati wa fainali za Euro 2012 |
RIO DE
JANEIRO, Brazil
PELE
anaamini kwamba sasa ni wakati muafaka kwa kipa Iker Casillas kupewa tuzo ya
Mwanasoka Bora wa Dunia (Ballon d'Or) kufuatia kiwango chake cha juu
alichoonyesha wakati akiidakia timu yake ya taifa ya Hispania katika fainali za
Euro 2012.
Pele |
Nahodha huyo
mwenye miaka 32 alienda katika fainali hizo baada ya kuisaidia klabu yake ya Real
Madrid kutwaa ubingwa wa La Liga, Ligi Kuu ya Hispania msimu wa 2011-12, na
aliruhusu goli moja tu katika fainali za Euro zilizoandaliwa na Poland na
Ukraine wakati Hispania ikitwaa tena ubingwa.
Pele
anaamini kwamba makipa wamekuwa wakisahaulika katika miongo michache iliyopita
wakati akisifia kiwango cha Casillas kwenye michuano mikubwa, na kutaka apewe
tuzo hiyo badala ya Lionel Messi.
"Kwa
kawaida, ni washambuliaji (wanaopewa tuzo ya Ballon d'Or), lakini mimi naamini
haitakuwa sawa kutoa tathmini yangu kwa vile sijaona mechi zote," Pele
aliiambia AS.
"Hata
hivyo, bado hakuna shaka yoyote kuhusiana na kiwango cha Casillas kwenye
michuano mikubwa. Hii ndio fursa nzuri
zaidi, ndio wakati muafaka wa yeye kupewa tuzo ya Ballon d'Or.
"Amechangia
kwa ushindi kwa kiasi kikubwa kama walivyofanya washambuliaji. Unaweza kuwa na
No.10 bora kabisa, lakini asiwe na msaada wowote kama hakuna kipa bora nyuma
nyuma yake.
"Nilikuwa
muhimu sana (kwa Brazil), hilo sikatai, ni kwa sababu nilikuwa mshambuliaji.
Lakini waangalie (Amadeo) Carrizo, (Lev) Yashin and (Gordon) Banks. Watu
hawazungumzii makipa."
.... ASIKITIKA LIONEL MESSI KUKOSA MPINZANI
Pele pia
alizungumzia hali ya sasa ya mchezo wa soka wakati akielezea kukosekana kwa
ushindani wa dhati katika ngazi ya Dunia dhidi ya Messi, kabla ya kulaumu
vyombo vya habari kwa tabia ya kuzidisha ‘misifa’ kwa wachezaji.
"Kila
zama zina nyota wake," alisema.
"Kuna wakati kunakuwa na wachezaji wanne
hadi watano wa kuwalinganisha, lakini kwa mtazamo wangu, sasa hivi hilo halipo.
"Nani
leo hii wa kumlinganisha na Messi? Neymar? Cristiano (Ronaldo) ni wa pili,
lakini nani mwingine wa kushindana naye?
"Vyombo
vya habari nd’o vinavyotengeneza tofauti. Nitapaswa kwenda na kucheza mwezini
ili kupata mafanikio niliyowahi kuyapata. Leo, kijana anafunga bao kali na
dunia nzima inamtukuza."
No comments:
Post a Comment