TIMU za Kinondoni na Dodoma zimeingia robo fainali ya michuano ya Copa Coca
Cola 2012 baada ya kushinda mechi zao za 16 bora zilizochezwa leo jijini
Dar es Salaam.
Kinondoni
imeitoa Rukwa baada ya kuichapa mabao 3-1 katika mchezo uliofanyika
Uwanja wa Karume. Mabao ya washindi yalifungwa na Yahya Mohamed dakika
ya 13, Issa Allydakika ya 44 na Mabrouk Liyayala dakika ya 80. Ladislaus
Fwamba aliifungia Rukwa dakika ya 46.
Kwa
ushindi huo, Kinondoni itacheza robo fainali ya tatu Julai 10 mwaka huu
Uwanja wa Karume dhidi ya mshindi wa mechi ya 16 bora kati ya
Kilimanjaro na Mwanza itakayochezwa leo saa 10 jioni.
Nayo
Dodoma imenyakua tiketi ya kucheza robo fainali baada ya leo kuifunga
Arusha bao 1-0 katika mechi iliyochezwa Uwanja wa Tanganyika Packers.
Bao la washindi lilifungwa dakika tano kabla ya filimbi ya mwisho na
Ayoub Khalfan.
Katika
robo fainali, Dodoma itacheza na mshindi wa mechi ya 16 bora kati ya
Tabora na Tanga itakayochezwa leo jioni Uwanja wa Tanganyika Packers.
Robo
fainali zote zitachezwa Uwanja wa Karume ambapo ya kwanza itafanyika
keshokutwa asubuhi (Julai 10 mwaka huu) kati ya Temeke na Mjini
Magharibi wakati jioni itakuwa Mara na Morogoro.
No comments:
Post a Comment