Tuesday, July 3, 2012

KINA GOMEZ, OZIL, KHEDIRA WAPIGWA ZENGWE UJERUMANI


Gomez (katikati) akiwa mwenye huzuni tele baada ya kipigo walichopata kutoka kwa Italia.
Khedira

Mtazame Ozil anavyolia kwa uchungu baada ya kutolewa... eti ni kweli yeye na wenzake hawana uzalendo?
BERLIN, Ujerumani
NOTA wa timu ya taifa ya soka ya Ujerumani, ambao bado wanaugulia machungu ya kipigo cha 2-1 katika mechi yao ya nusu fainali ya Euro 2012 dhidi ya Italia wiki iliyopita, sasa wanashutumiwa vikali kwa kutokuwa wazalendo kutokana na kile kinachodaiwa kuwa ni kutoimba wimbo wa taifa.

Wachezaji wengi wa Ujerumani, wakiwemo Mario Gomez, Mesut Ozil, Bastian Schweinsteiger, Sami Khedira na Manuel Nuer wanadaiwa kuwa walibaki kimya wakati wimbo wa taifa lao ukipigwa uwanjani mjini Warsaw Alhamisi iliyopita,  huku wachezaji wote wa Italia wakionekana kuimba wimbo wao wa taifa kwa furaha.

Nchini Ujerumani, serikali za shirikisho huamua kama watoto wajifunze wimbo wa taifa wawapo shuleni ama la. Kinyume chake, kwa wahafidhina wa Bavaria ni lazima kujifunza wimbo huo, wakati mjini Berlin jambo hilo hutegemeana na uamuzi wa walimu wenyewe.

No comments:

Post a Comment